CHRISTIAN CHURCHES OF GOD
P.O.BOX 369 WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Coordinator-General: Wade Cox
E-mail: secretary@ccg.org
In North America
PO Box 1537, Blue
Springs, MO 64013-1537, United States of America
Copyright © 1994,1995,1996,1997, Christian Churches of God
Karatasi hii inaruhusiwa kunukuliwa na kusambazwa kwa yeyote mradi tu kama itanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kuondoa maana halisi. Jina la mchapishaji na anuani yake na tangazo la hati miliki lazima vijumlishwe. Hakuna gharama yoyote ipaswayo kuchangiwa na mtumiaji na hairuhusiwi kuuzwa nakala zake kwa msomaji. Nukuu chache zaweza kuchukuliwa katika makala zinazo tofautiana kimtazamo na kimaoni bila kukiuka maadili ya haki miliki.
Utangulizi
Sura 1. Uungu
1.1 Mungu Baba
1.2 Yesu Mwana wa Mungu
1.3 Roho Mtakatifu
1.4 Uhusiano kati ya Roho Mtakatifu, Kristo na Binadamu
1.5 Uhusiano kati ya Kristo, Shetani na Jeshi la Mungu
1.5.1 Kristo kama Mwana wa Mungu
1.5.2 Mafundisho ya mpinga Kristo
1.5.3 Jina na Ukuu wa Mungu
Sura 2. Mpango wa Wokovu
2.1 Anguko la Mwanadamu
2.2 Wokovu wa Mwanadamu
2.3 Biblia Kama Ukweli ulio Vuviwa
2.4 Kutubu na Kuongoka
2.5 Ubatizo
Sura 3. Mafundisho Kuhusu Wajibu wa
Mwanadamu
3.1 Maombi na Kuabudu
3.1.1.Mungu Kama Mlengwa apaswaye Kuombwa na kuabudiwa
3.1.1.1 Lengo La Maombi
3.1.1.2 Lengo La Ibada
3.1.1.3 Maombi ya Binafsi na ya wengi Kwaniaba ya Wengine
3.2 Uhusiano Kati ya Wokovu na Sheria
3.2.1 Mungu ndiye Mwamba wetu
3.2.2 Wokovu Kwa Neema
3.2.3 Ulazima wa kuwa chini ya Sheria
3.2.3.1 Kwanini ni lazima Wakristo washike Sheria
3.2.3.2 Wakristo kama Hekalu la Mungu
3.2.4 Amri Kumi
3.2.5 Sheria Nyingine zitawalazo Mwenendo wa Mwanadamu
3.2.5.1 Sheria ya Vyakula
3.2.5.2 Sabato
3.2.5.3 Mwandamo wa Mwezi
3.2.5.4. Siku Takatifu za Mwaka
3.2.5.5. Ndoa
3.2.6 Uwakili wa Mali
3.2.6.1 Kwaajili ya Mungu
3.2.6.2 Kwaajili ya Wengine
3.2.7 Mambo ya Vita na Uchaguzi
3.2.7.1 Vita
3.2.7.2 Uchaguzi
Sura 4. Mafundisho Kuhusu Masihi
4.1 Kuwepo kwa Kristo tangu Mwanzo
4.2 Kusulibiwa na Kufufuka
4.3 Kuja kwa Kristo Mara ya Pili
4.4 Utawala wa Milenia
Sura ya 5. Matatizo ya Uovu
5.1 Kuwepo kwa Uovu baada ya Uasi
5.2 Fundisho Kuhusu Kuchaguliwa Tangu Mwanzo
5.3 Hali ya Wafu
5.4 Ufufuo wa Wafu
5.5 Hukumu ya Waovu
Sura
6. Kanisa
6.1 Je,Kanisa ni nani au ninini?
6.2 Kanisa kama Shirika
6.3 Makusudio na Malengo ya Kanisa
6.4 Utakaso
Sura 7. Ufalme wa Mungu
7.1 Kuanzishwa kwa Ufalme wa Mungu
7.1.1 Ufalme wa Kiroho
7.1.2 Utawala wa Milenia wa Kristo
7.1.2.1 Kurudi Kwa Masiha
7.1.2.2 Kutaniko La Israeli
7.1.2.3 Siku ya Bwana
7.1.3 Utawala wa Milele wa Mungu
7.1.3.1 Ujio wa Mungu
7.1.3.2 Dunia Mpya na Yerusalem mpya
7.1.3.3 Hatima ya Wanadamu
Maongezo
Utangulizi
Kwa muda wa miaka mia saba, Ukristo umefungwa katika mfumo wa Teolojia ambao umeshikilia Falsafa za Kiyunani na mfumo shirikishi na fikra za Kiplatoni mamboleo. Mbinu za ki Unitariani za kupelekea Ujumbe wa Biblia na ukiambatana na ufunuo wa Mungu kwa mwanadamu katika Maagano yote imebadilishwa na kutumiwa kwa maslahi ya kuendeleza nguvu na mamlaka ya kiutawala ya Dunia.
Hatimaye matokeo yake ni kile kilichoeleweka kuwa ni muundo ulio anzishwa na braza la Nikea (451AD), Laodikia (366AD), Costantinopo (381AD), na Kalkedoni (451AD). Mfumo huo ulibadili mwelekeo wa Mungu kuhusu mlolongo wa kinasfi hatimaye kukaanzishwa imani ya Utatu. Baraza la Laodikia (canon 29) vilevile liliondoa Sabato na badala yake vikaingizwa na kukubalishwa sikukuu za Kipagani kutoka ibada za Jumapili hadi Mwezi Desemba sikukuu ya Juana mfumo wa Easter mahali pa Pasaka. Kingine kilichokuwa kimebadilishwa, ni jinsi ya kuelewa mfumo wa Kibiblia na kwamba sheria zilipaswa zitafsiriwe. Sheria zilizotolewa na Musa zikachukuliwa kuwa zimepitwa na wakati na maandiko ya Agano Jipya yakatafsiriwa vibaya ili yaunge mkono uwepo wa matendo ya kipagani.
Kwa mfano, Sheria ya vyakula ikaondolewa kwa kunukuu vibaya Matendo ya Mitume 10 na aya nyinginezo. Madhara katika afya ya mwanadamu yakaonekana maramoja. Hatahivyo, matokeo ya mwisho ya mazingira yalianza kuonekana kwa hakika baada ya miaka elfu mbili hivi. Uvunjaji wa kanuni za utaratibu wa vyakula vilichangia pia kwa kiasi kikubwa sana, kwaajili ya ulaji wa vyakula vilivyo katazwa chini ya Sheria za Kibiblia.
Mmomonyoko wa mfumo wa ardhi unaweza kuonekana kikamilifu baada ya ardhi inapokuwa imechoka kwaajili ya kushindwa kuadhimisha mfumo wa Jubilee na sabato za ardhi kwasababu walizivunja na na kufuata mfumo wa kalenda zenye mzunguko wa miezi kuminatisa. Kuanzishwa kwa mfumo wa kalenda za jua (solar) ilikuwa yenyewe tu ni hatua kubwa sana katika kuharibu isieleweke mfumo na mzunguko ambao Mungu aliuweka kwa jinsi ya mpangilio wa asili.
Ukristo uliopo leo kwa wingi au kwa uchache haufanani na ule Ukristo wa asili wa zamani. Kuibuka kwa Uislam na vita vya baadae na waislam kulikuwa ni matokeo dhahiri ya mfumo wa Ukristo wa uwongo ulioanzilishwa na Ulaya na Asia Magharibi na mfumo wa falsafa za Kiyunani kwa kutumia teolojia ya Wakapadokiani iliyoamini Mungu wa nafsi Tatu na kwamba kuna mahusiano ya siri na Mungu na ni ndio Mungu. Mfumo huu wa ki-Utatu hauwezi kufanya kazi. Matokeo ya mwisho ya miaka elfu moja na mia saba ya mafundisho haya ya uwongo yamekuwa ni kukaribia uharibifu wa Sayari na kuteswa kwa watu ambao wanajaribu kwa dhati ya moyo kutii sheria za kibiblia.
Madhumuni ya kazi hii ni kuutoa kwa uwazi na kwa njia rahisi iwezekanavyo ujumbe halisi wa Biblia na wa Kanisa la Agano jipya chini ya Yesu Kristo na Mitume. Bilashaka baadhi ya mambo yaliyo elezewa ndani yake yataleta changamoto na yatafishwa. Kazi imeandikwa ili kwamba iwe karibu iwezekanavyo, mafuatano ya maelezo ya kibiblia au mafafanuzi ambayo yanapata uungwaji mkono na aya zilizo nukuliwa. Kwa njia hii inachukuliwa kwamba kitabu hiki kimekamilika bila kutumia lugha za mafumbo na malengo yetu yako wazi kabisa. Ilipowezekana sehemu nyingine vitabu vingi vya biblia vimeorodheshwa ili kuepukana na nukuu chache. Baadhi ya aya za biblia zimekosewa kiuwazi kabisa. (mf. 1Jn. 5:7 KJV; 1Tim 3:16 KJV; kutokana na Codex A), au zingine zimetafsiriwa visivyo (mf. 1Kor.15:28 RSV, kadhalika Ufu.3:18 NIV ni baadhi tu ya zile zingine), zilifanywa hivyo ili ziunge mkono fundisho la Utatu au mfumo wa Wakapadokiani vinavyotaka kuonekana haviendani.
Wakati Masihi ajapo tena atakuja kurudisha tena mfumo wa sheria alizompa Musa pale Sinai.Kila Mkristo anao wajibu kudhihirisha na kuendeleza mfumo wa jinsi ya kuishi na na kuabudu sawa na ilivyo elekezwa katika Biblia. Makristo analazimika kujitahidi kupita njia ya maisha Yesu Kristo na kuishi katika mfumo ule ambao Kristo alifundisha na alivyoishi kama mwanadamu na aliyetoka juu. Kitabu hiki kimetolewa ili kuelezea mfumo mzima wa jinsi tunavyoishi kwa nia ya kutulinda na mfumo wa uwongo mpotofu na mfumo ule ambao kwa miaka elfu moja na mia saba utupiliwe mbali na njia halisi nay a kweli iweze kujulikana na ianze kufanya kazi ndani ya maisha ya watu haijaliishi nini walifanya nini huko nyuma. Jukumu letu ni kuwaita watu kwenye toba na upya wa uzima.
Sura ya 1
Uungu
1.1 Mungu Baba
Nafasi ya juu sana Ulimwenguni iliyo bora na kutukuka sana kwahabari ya mambo ya Uungu ni ya Mungu. Yeye ndiye mwenge nguvu zote, Muumbaji na na mwenye kuvifanya viendelee kuwepo Mbingu, dunia na vyote vilivyomo ndani yake (Mwa.1:1; Neh.9:6; Zab.124:8 Isa.40:26,28; 44:24; Mdo.14:15; 17:24-25; Ufu.14:7). Yeye pekee ndiye mwenye kuishi milele bila kufa (1Tim. 6:16). Yeye ndiye Mungu na Baba yetu, na pia ndiye Mungu na Baba wa Yesu Kristo (Yoh. 20:17). Yeye ndiye Mungu aliye juu sana zaidi vitu vyote (Mwa. 14:18; Hes.24:16; Kum.32:8; Mk.5:7) na ni Mungu wa pekee wa kweli (Yoh.17:3; 1Yoh.5:20).
1.2
Yesu Mwana wa Mungu
Yesu ni mzaliwa wa kwanza (proototokos) katika uumbaji (Kol. 1:15) yaani kuanzia mwanzo (arche) wa uumbaji wa Mungu (Ufu.3:14). Yeye ndiye mzaliwa pekee (monogene) Mwana wa Mungu (Mat. 3:17; Yoh. 1:18; 1Yoh. 4:9), aliyetungiwa mamba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu akazaliwa na bikira Mariamu (Lk. 1:26-35). Yeye ndiye Kristo au Masihi (Mat. 16:16; Yoh.1:41), aliyetumwa kutoka kwa Mungu awe Mwokozi na Mkombozi wetu (Mat.14:33; Yoh.8:42; Efe.1:7; Tit.2:14). Anaitwa ni Mwana wa “Mungu aliye juu sana” (Mk. 5:7). Alikuwa ni Mwana wa Mungu aliyekirimiwa uweza wa Roho ya Utakatifu na kufufuliwa kutoka mautini (Rum.1:4). Emepewa kiti cha enzi cha Daudi ili kutawala nyumba ya Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho (Lk. 1:32).
1.3
Roho Mtakatifu
Roho Mtakatifu (Mdo. 2:4) ni kiini au nguvu za Mungu ambaye Kristo aliahidi kumtuma kwa wateule (Yoh.16:7). Yeye siyo nafsi au mtu, lakini ni mgawanyo tu wa nguvu za Mungu zilizo hai. Ni kwakupitia yeye sisi tunafanyika kuwa warithi wa Asili ya mambo ya Mbinguni (2Pet. 1:4), kujazwa na Roho Mtakatifu (Mdo.9:17; Efe.5:18) na hivyo sote kufanyika watoto wa Mungu (Ayu.38:7; Rum.8:14; 1Yoh.3:1-2) na warithi pamoja na Kristo (Rum.8:17; Gal.3:29; Tit.3:7; Ebr.1:14, 6:17, 11:9; Yak.2:5; 1Pet.3:7) Hutolewa na Mungu kwa wale wamuombao (Lk.11:9-13) na wanao mtii, Hukaa ndani yao wale wanazishika Amri za Mungu (1Yoh.3:24; Mdo.5:32). Roho Mtakatifu ni mfariji ambaye huwaongoza watumishi wa Mungu na kuwatia katika kweli yote (Yoh. 14:16,17,26). Roho Mtakatifu hutia nguvu za kushuhudia (Mdo.1:8). Hushughulika na maongozi ya karama kama zilivyo elezewa katika 1Wakorintho 12:7-11 na anayo matunda kama ilivyoelezewa katika Wagalatia 5:22-23, hatolewi kwa kipimo (Yoh. 3:34 RSV; Rum.12:6) Kwakupitia yeye hatimaye Mungu hufanyika ni yote katika yote (1Kor.15:28; Efe 4:6).
1.4 Uhusiano kati ya Roho Mtakatifu, Kristo na Binadamu
Roho Mtakatifu hufanya kazi kwa mtu hata kabla ya Ubatizo. Roho humleta mtu binafsi yake kwa Mungu kupitia Kristo (Ebr. 7:25)
Matunda ya kwanza ya Roho hutolewa kwa mwanadamu pale anapobatizwa, kama isemavyo Warumi 8:23, ambapo inasema waziwazi kuwa kufanyika mwana hakutimiliki hadi ukombozi wa mwili.
Hivyo basi tumezaliwa mara ya pili lakini tunaendelea kukua katika Roho kila siku katika Kristo Yesu hadi kuufikia utukufu wa Mungu. Roho Mtakatifu ni Roho wa Mungu (Rum. 8:14) na ni Roho wa imani (2Kor. 4:13) ambaye huchunguza mambo yote na hufahamu mambo yote (1Wak.2:10-11, 12:3ff.).
Hivyo basi, Roho Mtakatifu siyo kuwa ni kitu kinacho jitegemea cha Mungu mwenye mfumo wa Utatu, lakini ni njia ambayo sisi tumefanyika kuwa ni elohim (Zek. 12:8). Roho huwakilisha kwa Mungu uelewa wa mawazo yetu na uanadamu wetu, tukiwezeshwa kupitia Yesu Kristo kama mwombezi na mpatanishi wetu yaani elohim au theos (Zab. 45:6-7; Zek.12:8; Ebr.1:8-9) anamuwezesha Kristo kutusaidia, kutufundisha na kutufariji na kutuwezesha kuzifanyia kazi nguvu za Mungu. Roho hutoa kwa kila mtu tabia njema kama apendavyo Mungu ili kuufaidia mwili wa Kristo kama inavyosema 1Wakorintho 12:7-11.
Roho anaweza kuzimwa (1The. 5:19) kwa kukataliwa au kwa kuhuzunishwa (Efe. 4:30) hivyo basi aweza kuona faida na hasara katika nafsi ya mtu.
Tunda la Roho Mtakatifu ni Upendo kama isemavyo wagalatia 5:22. Hivyo basi, kama hatupendani sisi wenyewe Roho Mtakatifu hayupo mahali hapo.
Roho ni njia ambayo kwayo kwayo kwayo tunamuabudu mungu kama inavyoelekezwa katika Wafilipi 3:3. hivyo basi hawezi kuwa Mungu kiasi cha kuwa mlengwa katika ibada kiasi cha kuabudiwa na hivyo kuwa sawa na Mungu Baba. Ni nguvu imtiayo nguvu Kristo. Pale isemwapo kuwa Kristo ni Baba wa Milele, (Isa. 9:6) ni kwamba kuna aina nyingi ya ubaba mbinguni na duniani (Efe. 3:15). Kristo amefanyika kuwa Baba wa Milele kwa njia ya uwakilishi.
Aina hizi zote za ubaba au familia zimetumika kumtaja Mungu Baba hii ndiyo maana tunapiga goti mbele zake Mungu Baba na kumuabudu (Efe. 3:14-15).
Kristo mzaliwa wa kwanza au mzaliwa wa kwanza katika Uumbaji. Kwakuwa katika yeye viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni viti vya enzi,au usultani, auenzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwaajili yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye. (Kol. 1:16-17). Lakini ilikuwa ni Mungu aliye mfanyiza na aliyerithia kwmba uumbaji udumu na uwepo katika Kristo. Hivyo basi, Kristo siyo Mungu kwa namna yeyote ile kama Mungu Baba alivyo Mungu na kwamba yeye tu pekeyake mwenye kuishi milele bila kufa (1Tim. 6:16) huishi bila kutegemea kitu chochote katika umilele.
Wakristo wameitwa kutoka katika dunia hii ili waishi maisha ya utumishi na kujitoa wakfu. Walioitwa ni wengi lakini wateule ni wachache (Mat. 20:16, 22:14). Wakristo ni watu waliochaguliwa kama vile Kristo alivyokuwa amechaguliwa na Mungu (Lk. 23:35). Wateule wamechaguliwa na Kristo (Yoh. 6:70, 15:16,19), kwa maongozi ya Mungu. (1Pet. 2:4).
Ili kulisaidia Kanisa, wateule ambao ndio Kanisa au ecclesia, wamepewa majaliwa ya kuzijua siri za Mungu. Roho Mtakatifu ndiyo anayefanya kazi hiyo ya kuwawezesha kuelewa siri za Mungu na za Ufalme wa Mungu (Mk. 4:11). Kwakuwa hekima ya Mungu huongelewa kwa njia ya mafumbo (1Kor. 2:7), ambayo hutafafanuliwa na watumishi wa Mungu (1Kor. 2:7, 15:51). Kwakuwa mapenzi ya Mungu yameelezewa kwa njia ya mafumbo (Efe. 1:9) ambayo Mungu aliwapa watumishi wake kwa njia ya ufunuo . Zaidi ya yote, siri hizo ziko katika utumishi wa Kristo kupitia wateule. Mtume Paulo aliandika:
…ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwaajili yenu; ya kwamba kwakufunuliwa nalijulishwa siri hiyo, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.Kwahayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo. Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho; ya kwamba Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmoja, na wa mwili mmoja na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili; (Efe. 3:2-6).
1.5 Uhusiano Kati ya Kristo, Shetani na Jeshi la Mungu
Kuna aina mbalimbali ya matumizi ya neno Elohim au Theoi lilivyo tumika katika Biblia likitumiwa kwa maana ya miungu. Kristo ni miongoni mwa watu wanaoonekana kutujumuishwa katika kundi hili katika rejea za Agano La Kale kama Elohim (tazama Zek.12:8). Kristo anatajwa tena katika rejea za Agano Jipya kama ni Nyota mpya ya Afajiri katika kurudi kwake duniani. Atawashirikisha daraja hili la heshima wateule wake (Ufu. 2:28, 22:16).
Mungu anasisitizwa katika Biblia kuwa ni Mungu na Baba wa Kristo (soma Rum.15:6; 2Kor.1:3, 11:31; Efe.1:3, 17; Kol.1:3; Ebr.1:1 ff; 1Pet.1:3; 2Yoh.3; Ufu.1:1,6, 15:3) Kristo alitoa uhai wake, nguvu na mamlaka kwa amri ya Mungu Baba (Yoh.10:17-18). Kristo aliyatiisha mapenzi yake yaendane na vile Mungu alipenda ambaye ni Baba (Mat. 21:31, 26:39; Mk.14:36; Yoh.3:16, 4:34). Mungu amempa Kristo wateule wote kuwa wake na Mungu ni mkuu kuliko Kristo (Yoh. 14:28) na ni mkuu kuliko vitu vyote (Yoh.10:29). Hivyo basi, Mungu alimtuma mwanawake wa pekee (monogene) duniani ili sisi tuishi kupitia yeye (1Yoh. 4:9). Ni Mungu ndiye ampaye heshima na kumtukuza Kristo (Yoh. 8:54), Mungu akiwa ndiye mkuu kuliko Kristo (Yoh. 14:28).
Mungu ni Mwamba (sur) kama Jabali au Mlima ambalo wengine wote wametokana kwayo, jiwe la gumegume la Yoshua 5:2 lililo watahiri Israeli, kanuni na sababu kuu muhimu (Kum. 32:4). Mungu ndiye Mwamba wa Israeli, Mwamba wa wokovu (Kum. 32:15), Mwamba ule uliowazaa (Kum. 32:18,28-31). 1Samweli 2:2 hutuonyesha kuwa Mungu wetu ndiye Mwamba wetu, Mwamba wa milele (Isa. 26:4). Ni kutokana na Mwamba huu ndipo wengine wote wametokea kama wote ni wana wa Abraham kwa njia ya imani (Isa. 51:1-2). Masihi ametokana na katika Mwamba huu (Dan. 2:34,45) ili kuzitiisha tawala zote za dunia. Mungu ni Mwamba au timazi ambayo msingi umewekwa na ambapo Kristo atalijenga kanisa lake (Mat. 16:24) na ambapo yeye mwenyewe huweka makao na kupumzika. Masihi ndiye Jiwe Kuu la Pembeni la Hekalu la Mungu, ambalo wateule ni Naos au Patakatifu pa Patakatifu, wakimtuinia Roho Mtakatifu. Mawe yote ya Hekalu yametokana ndani ya Mwamba ambao ni Mungu, kama ilivyokuwa kwa Kristo, na wamekabidhiwa kwa Kristo, mwamba war oho (1Kor. 10:4), jiwe likwazalo, na mwamba uangushao; (Rum. 9:23) ili kujenga Hekalu.
Kristo analijenga Hekalu ili Mungu awe yote katika yote (Efe. 4:6). Mungu amemfanya Kristo kuwa ni yote katika yote (panta kai en pasin Kol. 3:11) akivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake (1Kor.15:27) akimfanya wewe kuwa ni kichwa juu ya mambo yote katika Kanisa ambalo ndio Mwili wake, utimilifu wake ambao unaokamilisha mambo yote katika yote (Efe.1:22-23).Wakati Mungu alipo vitiisha vitu vyote chini ya Kristo, ilikuwa inaashiria kuwa Mungu alimteua yeye mwenyewe ili avitiishe vitu vyote chini ya miguu ya Kristo (1Kor. 15:27).
Wakati Kristo anapovitiisha vitu vyote ndipo hatimaye Kristo mwenyewe atajitia chini ya Mungu aliye vitiisha vitu vyote kwa Kristo ili Mungu awe yote katika yote (panta en pasin 1Kor. 15:28 sio sawa na vile tafsiri ya RSV). Hapa ndipo mafundisho ya Waplatoni yanapotafuta kuchanganyisha kati ya Mungu na Kristo katika maandiko yanayojichanganya kuhusu Utatu. Kristo atakaa mkono wa kuume wa Mungu, kwa maongozi ya Mungu (Ebr. 1:3, 13, 8:1, 10:12, 12:2; 1Pet.3:22) ambacho ni kiti cha enzi cha Mungu (Zab.45:6-7; Ebr.1:8) au Mungu yuko juu ya kiti chake cha enzi imetafsiriwa kuwa kiti chako cha enzi ee Mungu (angalia rejea za chini “footnote” katika Biblia ya RSV).
Mungu, ambaye anatuma ni mkuu kuliko yeye anayetumwa (Yoh. 13:16), mtumwa hawi mkuu kuliko Bwana wake (Yoh.15:20)
Kristo alishindana na Shetani na kukutana na majaribu makuu ambayo Shetani aliyaandaa. Shetani ambaye alikuwa ni Nyota ya Asubuhi, Lusifa au mleta nuru katika dunia hii (Isa. 14:12) kama alivyokuwa mlinzi na mwalimu, kikamilifu kabisa, mmoja kati ya Elohim ambaye alikuwa chimi ya Mungu Baba.
Kristo alikuwa ndiyo ambayo ilikuwa itokee katika nyumba ya Yakobo (katika Hesabu 24:17). Hivyo basi, iliashiriwa katika Vitabu vya nabii Musa kuwa mojawapo ya Nyota ya Asubuhi ambayo imetajwa kuwa itakuwepo katika mwisho wa hii sayari hii (katika Ayubu 38:7), mmojawapo wa elohim, alipaswa afanyike kuwa mwanadamu katika Yakobo na katika Daudi (Ufu.22:16).
Huyu elohim tumjuaye kama Yesu Kristo alikuwa bado sio Nyota ya Asubuhi ya sayari hii. Cheo kilishikiliwa na Shetani (soma Isa.14:12 na Eze.28:2-10).
Kristo alipakwa mafuta kuwa ni elohim wa Israel usomapo Zaburi 45:7 na mpakwa mafuta juu ya washiriki wake au watendakazi pamoja naye. Hata hivyo, Kristo kwakweli hakuwa katika cheo cha kuwa Nyota ya Asubuhi na hataweza kuzifanya kazi hizo hadi pale atakapo rudi mara ya pili. Cheo na majukumu ilipaswa vishirikishwe kati ya Kristo na wateule, ambao wamejumuishwa katika asili yake kama Nyota ya Asubuhi katika mioyo yao (imetafsiriwa kama Nyota ya Mchana katika 2Pet.1:19). Wateule wameahidiwa kushirikishwa katika uweza huu usomapo Ufunuo 2:28.
Shetani, kama Nyota ya Asubuhi, alishindana na Mungu Mkuu Aliye juu sana au Mungu Baba kama tunavyoambiwa katika Isaya 14:12. Alijaribu kujikweza au kukiinua kiti chake cha enzi, kiti cha enzi cha Mungu, juu ya Nyota za Mungu au baraza la Elohim. Baraza hili ni Kusanyiko la Elohim au Miungu kama inavyosema Zaburi 82:1. Ni jambo la kufurahisha sana kufahamu kuwa Irenia mwanafunzi wa Polycarp, mwanafunzi wa Mtume Yohana, alishikilia kwamba Zaburi 82:1 inapelekea kwa Theoi au miungu ambayo ilijumuisha vilevile wateule, kwa jina la wale waliofanywa wana (kinyume na Mafundisho Potofu ‘Heresies’, Bk.3, Ch.6, ANF, Vol.1, p.419).
Kuna aina mbalimbali ya Wana wa Mungu (kulingana na Ayubu 1:6, 2:1, 38:7; Zab.86:8-10, 95:3, 96:4, 135:5) waliojulikana kama Bene Elyon au Wana wa aliye juu sana. Binadamu wateule vilevile wamejumlisha pamoja na Jeshi la mbinguni kama Wana wa Mungu (Rum. 8:14). Hivyo basi Kristo na wateule kama Wana wa Mungu ni wamoja na Mungu kupitia Roho Mtakatifu, waliokusudiwa tangia mwanzo wa kuwekwa misingi ya dunia. Kristo aliachia chini uweza wake na kufanyika kuwa mwanadamu. Yeye pamoja na wateule wote wamepokea Uwana kwa uweza kulingana na Roho ya Utakatifu kwa kufufulika kwake kutoka na nguvu za mauti (Rum. 1:4).
Katika Matendo 7:35-39 alikuwa ni malaika aliyesema na Musa katika mlima wa Sinai na malaika huyo ni Kristo. Katika wagalatia 4:14 Paulo hujifananisha na malaika wa Mungu vilevile Yesu Kristo.
Vilevile sisi tutakuwa kama malaika (Mat. 22:30) kama amri au isaggelos (Lk. 20:36) kuwa warithi pamoja na Kristo (Rum. 8:17; Gal.3:29; Tit.3:7; Ebr.1:14, 6:17, 11:9; Yak.2:5; 1Pet.3:7). Agano la Kale linamtaja malaika wa YHWH kwa namna zote Yehova na Elohim (Kut. 3:2,4-6 wakati Mungu au elohim hapa alikuwa ni malaika; mfano Zek.12:8).
Zabiri 89:6-8 hutuonyesha kuwa kuna Baraza la Watakatifu (qedosim au qadoshim, vilevile imetumika kama wanadamu) hujumlishwa na yote mawili baraza la ndani na la nje. Hii inajulikana kuwa ni Baraza la kimbinguni la Elohim wa haki.
1.5.1 Kristo kama Mwana wa Mungu
Shetani alipania kumjaribu Kristo kwa njia mbalimbali. Kwanza kabisa shetani alimtaja yesu kama Mwana wa Mungu (Mat.4:3, 4:6; Lk.4:3). Mapepo pia walimtaja Kristo kama Mwana wa Mungu (Mat. 8:29; Lk.4:41; Mk.3:11). Shetani aliojaribu kumfanya Kristo athibitishe sehemu yake kama Mwana wa Mungu kwa njia ya kutumia vibaya mamlaka yake, kwakuwa Mungu aliahidi kuwa atamtumia malaika zake wamlinde (Zab. 91:11-12). Shetani akaruka pale inaposema kukulinda katika njia zako zote na akaongeza neno wakati wote. Hivyo basi kwa njia hii ya kupindisha maandiko Shetani alikuwa anajaribu kuchukua uhai wa Kristo.
Kristo hawa mara moja hakumsahihisha Shetani wala mapepo kwa kudai yeye alikuwa ni Mungu badala ya Mwana wa Mungu. Kwahakika, hakuna pepo aliye wahi kudai udanganyifu wa kuwa Kristo alikuwa Mungu Mkuu bora kabisa mpaka baada ya kifo chake na nia yake ilikuwa ni kuanzisha fundisho linalosema kuwa Kristo alikuwa Mungu katika namna moja ya kwamba Mungu Baba ni Mungu na kwamba amekamilika baada ya kifo chake, ni udanganyifu ambao Kristo angeukanusha maisha. Katika kila jaribu moja nia ilikuwa kudhoofisha utii wa Kristo kwa Mungu na kwa ile nia yake njema ili avunje maandiko. Shetani alikuwa anajaribu kumfanya Kristo amuabudu yeye. Alimuahidi Kristo kumpa utawala wa dunia hii iwapo tu kama Kristo angekubali kumuabudu.
Kristo hakubishania haki yake ya kutawala hii dunia au kuwa kwakweli yeye alikuwa ni mtawala. Badala yake Kristo alijibu:
…imeandikwa Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
Kristo hakumwambia Shetani kuwa ilpaswa Shetani amsujudie Kristo lakini badala yake alimpeleka kwenye nukuu za vitabu vya sheria. Kristo katika hatua yoyote ya huduma yake kamwe hajadai wala kujitangaza kuwa yeye ni Mungu. Alisema kuwa yeye ni Mwana wa Mungu. Na ni kwasababu hii ndiyo ilimfanya kuingia matatani.
Ni kama vile ilivyoandikwa katika Mathayo 27:43
Alimtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu’.
Hapa ndipo Kristo alipolia ili kutimiliza andiko katika Zaburi 22:1
Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?
Kristo ni dhahiri kabisa hakujiita wala kujichukulia mwenuewe kuwa ni Mungu. Kutia dhana hii kuwa yeye alikuwa ni sehemu ya uungu kwamba alidai hivyo na kuwa yeye yuko cheo sawa, ni ujinga.
1.5.2
Fundisho la Mpinga Kristo
Fundisho la Mpinga Kristo limeelezewa katika 1Yohana 4:1-2. Kulingana na maandiko yaliyoko katika Gombo halisi za zamani, 1Yohana 4:1-2 kadiri ilivyo sanifiwa na Irenia, Sura 16:8 (ANF, Vol.1, fn. p. 443).
Hivyo basi mfahamuni Roho wa Mungu: Kila roho inayokiri kuwa Yesu Kristo amekuja katika mwili ni ya Mungu; na kila roho inayomtenga Yesu Kristo sio ya Mungu ni ya Mpinga Kristo.
Mwana historia mmoja aitwaye Socrates alisema (katika VII, 32, p. 381) aya hii changanywa na wale waliotaka kutenganisha ubinadamu wa Yesu Kristo kutoka katika uhali yake ya kimbinguni.
Kristo kama Mwana na siyo Mungu Mmoja wa pekee (Yoh.17:3).
Pia katika Luka 22:70, wakasema wote,Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu?
Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.
Alijulikana kama Mwana wa Mungu pia katika:
* Mathayo 27:54 ambapo inasema Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.
* Marko 1:1 inasisitiza Injili kuwa ni Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
* Luka 1:35 inaelezea kuwa Mtakatifu atakaye zaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
Kufahamu kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu, ni ufunuo kutoka kwa Mungu.
Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona, kwakuwa mwili na damu havikukufunulia hili; bali Baba yangu aliye Mbinguni. (Mat.16:16-17)
Vilevile Mathayo 11:27 inasema:
Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu, wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia.
Hivyo basi, Baba huwafunulia mambo watu binafsi na humpa Kristo watu hao ambaye hatimaye huwafunulia Baba watu hao.
1.5.3
Jina na Ukuu wa Mungu
Hakuna shaka yoyote kuwa Mungu ni mmoja na ni mkuu. Mithali 30:4-6 inatuonyesha jina la Mungu nanikuwa anaye mtoto.
Ninani aliyepanda mbinguni
na kushuka chini?
Ninani aliyekamata upepo na
makonzi yake?
Ninani aliyefunga maji ndani ya nguo yake?
Ninani aliyefanya imara ncha zote za nchi?
Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe, kama
wajua?
Kila neon la Mungu [ELOAH] limehakikishwa;
Yeye ni ngao yao wamwaminio.
Usiongeze neno katika maneno yake;
Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.
Biblia hujitafsiri yenyewe na jina la Mungu linaonyeshwa waziwazi ikifuatilia maelezo ya swali na ni wazi kuwa uungu sio kitu cha muunganiko wa vitu vingi pamoja kama vile Baba na Mwana, lakini zaidi sana ni kwamba anaye Mwana.
Zaidi ya yote, Agano jipya huelezea waziwazi kuwa ni Baba anayepaswa kuabudiwa. Kristo alimuonya Mwanamke Msamaria katika Yohana 4:21 kwamba saa inakuja ambayo hamtamuabudu Baba katika mlima huu (Samaria), wala kule Yerusalemu. Lakini kwa msisitizo kabisa anasema katika Yohana 4:23:
Lakini saa inakuja inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
Kristo anaelekeza hapa kuwa anayepaswa kuabudiwa hapa ni Baba na sio yeye mwenyewe. Hivyo basi tunaona kuwa ni kufuru kubwa kudai kuwa anayepaswa kuabudiwa hapa ni Kristo aliye inuliwa na itkuwa ni kwenda kinyume na Yohana 3:14 isemapo kuwa Mwana wa Adamu alipaswa kuinuliwa juu kama vile Musa alivyo muinua yule nyoka jangwani. Kusudi la kusulibishwa ilikuwa ni ili mwanadamu apate uzima wa milele, na sio ili hatimaye Kristo awe ndiye mlengwa katika kuabudiwa kama inavyo fundishwa kwa uwongo. Kutokana na mtazamo huu wa potofu, pia imedaiwa kwa namna potofu sana kuwa Wakristo wanaabudu mwili wa Kristo na damu yake wakati wanaposhiriki Ekaristi.
Eloah ni Mungu wa Agano la Kale na Hekalu na ni Mungu wa Yesu Kristo wa Agano Jipya. Hekalu lililokuwako Yerusalemu lilikuwa ni nyumba ya Eloah (Ezra 4:24; 5:2,13,15,16,17; 6:3,5,7,8,16,17; 7:23). Alikuwa ni Eloah wa Israeli (Ezra 5:1; 7:15), Eloah Mukuu wa Mbinguni (Ezra 5:8,12). Alikuwa ndiye mlengwa katika kumtolea na kupokea sadaka katika Hekalu (Ezra 6:10) mahali alipokuwa amelikalisha Jina lake (Ezra 6:12). Yeye ndiye aliye amuru ujenzi wa Hekalu (Ezra6:14) na kusimamisha kwa ukuhani ili kumtumikia yeye (Ezra 6:18; 7:24) na wafanye mapenzi yake (Ezra 7:18). Torati ni Sheria za Eloah wa Mbinguni (Ezra 7:12-14). Wale wanaozijua sheria za Eloah walipaswa kuwafundisha wale wote wasiozifahamu (Ezra 7:25) na hukumu zilipaswa kufuata sheria za Eloah (Ezra 7:26). Anayetajwa hapa ni Baba ambaye ni Eloah mmoja na ni Mungu Aliye Juu Sana, Baba wa Masihi na wa watoto wa Mungu wote.
Sura ya 2
Mpango wa Wokovu
2.1 Anguko la Mwanadamu
Mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu na kufanana naye (Mwa. 1:26-27). Adamu na Hawa walilaaniwa kwasababu kutotii (Mwa. 3:16-19). Matokeo ya uasi huu, dhambi na mapatilizo ya mauti iliwapata wanadamu wote (1Kor. 15:22; Rum.5:12).
2.2
Wokovu wa Mwanadamu
Mungu hapendi mtu yeyote apotee (1Pet. 3:9). Ili kwamba mwanadamu aepukane na hukumu ya dhambi, Mungu aliandaa mpango wa wokovu ukihusisha na sadaka ya kifo na ufufuko wa Mwanae Yesu Kristo (Yoh. 3:16). Mpango huo ni kwa kutoa malimbuko ambayo ilikuwa ni Kristo ambaye ni malimbuko ya wote walio lala mautini (1Kor. 15:20). Mpango huu wa wokovu unaonekana kwa kioo kupitia Sikukuu takatifu za kila mwaka zilizoko katika Biblia (Law. 23).
2.3
Biblia kama Ukweli uliovuviwa
Kristo alisema: …imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu (Mat. 4:4; Lk.4:4). Biblia hujulikana kama Maandiko Matakatifu (Dan. 10:21), na yanayomuongoza mtu ili kuupata wokovu na madhihirisho ya nguvu za Mungu (Kut.9:16; Rum.9:17). Njia pekee ya kuupata wokovu ni Yesu Kristo (Rum.10:11) ambaye alitabiriwa na Maandiko Matakatifu kuanzia Musa na Manabii wengine (Lk.24:27), unabii katika Maandiko Matakatifu (Mat. 26:56; Rum.1:2). Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema (2Tim. 3:16).
Maandiko Matakatifu wakati wa Kristo na Mitume yalikuwa ni ya Agano la Kale tu (Mat. 21:42; Mk.12:10; Mdo 17:2). Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale ndiyo yaliyokuwa yanaoelezewa kuwa ni pumzi ya Mungu au yamevuviwa katika 2Timotheo 3:16. Agano Jipya ni nyongeza ya Agano la Kale. Halichukui nafasi mbadala ya Agano la Kale.
Agano la Kale liliandikwa siku za mapema zaidi likilenga kutupa maelekezo, ili kwamba kwa kusimama kwetu imara huku tukitiwa moyo na maandiko haya tupate tumaini (Rum.15:4). Kupotea ni matokeo ya kutoyajua Maandiko (Mat. 22:29; Mk.12:24). Watu wa Beroya waliyachunguza Maandiko kila siku, ili waone kuwa kama yale yanayosemwa ni ya kweli. Hali hii ilifanya waonekane kuwa ni wastaarabu (Mdo.17:11). Mtazamo mzima wa Biblia umechukuliwa kutokana na maeneo yote ya Maandiko Matakatifu, fundisho hadi fundisho, msitari hadi msitari (Isa. 28:10). Maandiko hueleza kuwa kwamba Yesu alikuwa Masihi au Kristo (Mdo.18:28). Ni Kristo kwa njia ya Roho Mtakatifu, anaye fungua ufahamu wa wateule akianzia na Mitume, ili kwamba Maandiko Matakatifu yaweze kueleweka. (Lk. 24:45).
Maandiko ya Agano la Kale lazima yatimizwe (Mat. 26:54,56; Mk.12:10; 14:49) na hayawezi kutanguka (Yoh.10:35). Maandiko mengi sana yalimuelekea na yalitimilizwa kwa Kristo au yata timilizwa na Kristo atakapo kuja mara ya pili (Ufu.1:7, 12:10, 17:14, 19:11-21), ambapo itakuwa katika uweza na utukufu (Mat. 24:30)
2.4
Kutubu na Kuongoka
Kwa Mwanadamu kuishi au kupata uzima wa milele, Mungu anahitaji ni sharti iwepo toba. Bila toba ni kuangamia (Lk.13:3-5)
Kristo alitumwa ili kuwaalika watu wote watubu (Lk. 11:32). Kristo alianza huduma yake baada ya Yohana Mbatizaji kutiwa gerezani (Mat. 4:12). Yohana alitiwa gerezani yapata baada ya Pasaka ya mwaka 28 BK (Yoh. 3:22-24, 4:12) ambayo ni Pasaka baada ya kuanzishwa kwa huduma ya Yohana katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio (Lk.3:1). Tangia wakati ule, Yesu alianza kuhubiri akisema Tubuni kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia (Mat. 4:17). Kristo akawatuma wanafunzi wake wakahubiri Injili ya toba, akiwapa mamlaka juu ya mapepo au roho chafu (Mk. 6:7,12; Lk.10:1,17-20).
Toba ilifundishwa kama ni kitu cha lazima katika kufutiwa dhambi (au madhaifu) (Matendo 8:22) ili kwamba wakati wa kujiburudisha awe akitokea kwenye uwepo wa Bwana, ili kwamba amtume Kristo aliye mchagua kwaajili yetu (soma pia Matendo 15:3).
Kanisa la Efeso waliambiwa watubu na kukumbuka pale walipoanguka, na kufanya kazi walizo fanya hapo mwanzo (Ufu. 2:5). Vilevile Kanisa la Pergamo liliambiwa litubu (Ufu. 2:16). Vilevile kama ilivyo kuwa Kanisa la Thiatira (Ufu. 2:21-22) ambalo mwana wa ukengeufu alitupwa juu ya kitanda chake na waalimu wa dini za uwongo. Kanisa la Sardi vilevile liliambiwa watubu vinginevyo Kristo angekuja kama vile mwivi ajavyo usiku na wao wasingeijua saa ya kuja kwake (Ufu. 3:19). Toba ndicho kitu kinachotiliwa mkazo kwa Makanisa yote ya Mungu, kama ni wajibu wa kwanza kabisa wa wote (Yak. 5:19-20).
2.5
Ubatizo
Mamlaka yote alipewa Kristo ikifuatiwa na ufufuko wake (Mat. 28:18). Aliwaamuru wanafunzi wake waende Ulimwenguni kote wakawafanye Mataifa yote kuwa wanafunzi na Kuwabatiza Katika Jina La Baba Katika Mwili wa Mwana Katika Nguvu za Roho Mtakatifu (Mat. 28:19). Na kuwafundisha kuyashika yote Kristo aliyo waamuru. Na kwamba atakuwa pamoja nao hadi ukamilifu wa dahari (Mat. 28:20).
Toba ni lazima iendane sambamba na Ubatizo vikiambatana na vipawa vya Roho Mtakatifu (Mdo. 2:38). Huwezi kumpokea Roho Mtakatifu hadi utubu na ubatizwe, ambako ni kuzaliwa mara ya pili. Usipo zaliwa mara ya pili huwezi kuuingia ufalme wa Mungu (Yoh. 3:3-5). Toba ni sharti lisiloepukika ili mtu abatizwe na kumpokea Roho Mtakatifu. Ndiyo maana ubatizo wa watoto hauna maana na ni kinyume kabisa cha vile Biblia inavyo sema. Toba yenye masharti ilisisitizwa katika huduma ya Yohana Mbatizaji ambaye alishuhudia mara moja ubatizo wa Roho Mtakatifu kwa Kristo (Mk. 1:4,8). Yohana alisema kuwa Kristo atawabatiza watu kwa Roho Mtakatifu na kwa moto, kuhusu wale wasiotubu (wameelezewa kama makapi) (Lk. 3:16-17), Roho Mtakatifu huwezeshwa kufanya maongozi ya Mungu. Kwa njia ya maombi, huonekana kwa njia ya kuwekewa mikono, Roho Mtakatifu humshukia mtu binafsi yale. Hivyo basi Roho huweza kufanya aina yoyote ya kazi njema. Roho Mtakatifu huanza kufanya kazi hata kabla ya ubatizo akishughulika na mtu binafsi. Roho huwaleta wateule kwa Kristo (Ebr. 7:25). Sehemu ya kwanza ya tunda la Roho atapewa muamini wakati ule wa ubatizo, kama isemavyo Warumi 8:23, ambapo inasema kuwa kufanywa wana hakukamiliki hadi pale ukombozi wa mwili. Hivyo basi, sisi tumezaliwa mara ya pili lakini bado tunaendelea kukua katika roho kila siku katika Kristo Yesu hadi tutakapo ufikilia utukufu wa Mungu.
Hali hii ya utendaji kazi wa Roho Mtakatifu wakati wa ubatizo ni maji ya kisima cha wokovu kama ilivyoahidiwa na Mungu kupitia manabii wake (Isa. 12:3). Maji haya ya Roho Mtakatifu ni ahadi ya Mungu kwa Yakobo kama ilivyoandikwa katika Isaya 44:3. Bwana Mungu ndiye chemichemi ya maji ya uzima (Yer. 2:13, 17:13; vilevile Zek.14:8) Huu ndio mto wa maji ya uzima (Ufu. 22:1). Kristo anaongelea kwa habari ya Roho (Yoh. 7:39), alisema kutoka kwake maji yaliyo hai hutiririka (Yoh. 4:10-14; 7:38 cf. Isa.21:3; 55:1; 58:11; Eze. 47:1) Israeli wamesafishwa kiroho katika maji kulingana na andiko la Ezekieli 36:25, ambaye ni maji ya uzima au Roho Mtakatifu. Wateule huchota maji haya bila kulipa kitu (Ufu. 22:17).
Sura ya 3
Mafundisho
Kuhusu Majukumu ya Mwanadamu
3.1 Maombi na Kuabudu
3.1.1 Mungu ipasavyo kuwa ni
mlengwa katika Kusifiwa na Kuabudiwa
3.1.1.1 Lengo la Kuabudu
Sehemu ya kwanza na kanuni inayo ashiria kwa mteule ni kwa wakati wote awe ni imani juu ya Mungu mmoja tu, imani ambayo chanzo chake ni mahusiano na Yesu Kristo. Tusiabudu Elohim mwingine zaidi ya Mungu (Kut. 34:14; Kum.11:16) vinginevyo tutaangamia (Kum 30:17-18). Mungu alitoa amri ya kwanza ikisema:
Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya Utumwa. Usiwe na Miungu (elohim) mingine ila mimi. (Kut. 20:2-3)
Wazo hapa kusema mbele yangu inamaanisha kuwa sambamba yaani kufanya kitu m’badala au bila mamlaka ya Mungu tunayemulewa kuwa ni Mungu Baba.
Tunapaswa kumpenda Bwana Mungu wetu na kumtumikia kwa mioyo yetu yote na kwa roho zetu zote, yaani kwakuwepo kwetu, ilituweze kupata vyua kwa yake tuweze kupata mazao na malisho kwa mifugo yetu. Kwa maneno mengine ni kwamba tutakula vitu vingi (Kum.11:13-15). Lakini tunalo Agano jipya ambalo Bwana anaweka Sheria zake katika nia zetu na kuziandika mioyoni mwetu. Yeye ndiye Mungu wetu na sisi ni watumishi wake, ili tumuabudu yeye, kwa kuzishika Sheria zake katika hali yetu hii tuliyonayo (Ebr.8:10-13).
Inapaswa kumuabudu Bwana Mungu wetu (Kum. 26:10; 1Sam.1:3; 15:25). Mungu huyu ni Mungu mmoja ambaye ni wapekee wa kweli ambaye ni Mungu Baba. Sharti la kuupate uzima wa milele ni kwamba, lazima tumjue yeye (Mungu) na Mwanae Yesu Kristo (Yoh.17:3). Tunampatia Bwana, utukufu wa Jina lake; tunamuabudu Bwana kwa uzuri na utakatifu (Zab. 29:2; 96:9). Dunia yote inamuabudu yeye na humwimbia nyimbo za sifa kulisifu Jina lake (Zab. 66:4). Huu ni unabii na utakuja timilika. Mataifa yote aliyoyafanya yatakuja kumsujudia, kwa kutetemeka mbele zake (Zab. 96:9), yakilitukuza Jina lake, kwakuwa yeye peke yake ndiye Mungu (Zab. 86:9-10), Bwana Muumbaji wetu. Yeye ndiye Mungu wetu sisi ni kondoo wa malisho yake (Zab. 99:5,9). Yeye ni Mtakatifu (Zab. 99:5,9). Kuelewa ni nani tunaye muabudu vilevile kumeonyeshwa katika ishara kuu mbili ambazo kwa pamoja na kuelewa asili ya Mungu kunako fanyiza kuwekwa muhuri kwa wateule. Alama hizo mbili ni:
1. Sabato (soma Kutoka 20:8,10-11; Kum. 5:12). Sabato ni ishara kati yetu na Mungu atutakasaye (Kut. 31:12-14); na
2. Pasaka. Pasaka ni ishara au muhuri ambapo katika Kutoka 13:9,16, Pasaka inajumlishwa na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, ni ishara ya sheria ya sheria ya Bwana (Kum.6:8) na alivyo wakomboa Israeli (Kum. 6:10) ambayo katika Agano Jipya, inamaanisha ni kwa wote walio ndani ya Kristo (Rum.9:6; 11:25-26).
Ishara hizi za sheria, Sabato na Pasaka, viliwekwa kwa makusudi kabisa ili kuwalinda na ibada za sanamu (Kum.11:16). Ishara hizi mbili ni muhuri waliogongwa wateule katika mikono yao na vipaji vya nyuso zao, na kwa Roho Mtakatifu, itakuwa ndio msingi katika kuwatia muhuri kwa wale watakatifu 140,000 wa siku za mwisho walioandikwa katika Ufunuo 7:3. Zinatuongoza kuelekea katika Siku takatifu za mwisho.
Kristo alisema: Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake (au kumtumikia) (Mat. 4:10; Lk.4:8). Vivyo basi kumtumikia ni kuabudu katika lugha ya Kibiblia.
Kumwabudu Mungu kwa nia ya kuonekana na watu ni ibada isiyo na maana (Mat. 15:8-9). Kwakuwa Baba hupendezwa watu wamwabudu katika roho na kweli (Yoh. 4:21-24). Kwakuwa sisi tu tohara ya kweli tumwabuduo Mungu katika roho na ukufu katika Kristo Yesu (Flp. 3:3). Baraza lote la wazee, pamoja na Kristo, humwabudu Mungu aliye viumba vitu vyote na ambaye kwa yeye vilifanyika na huishi (Ufu. 4:10). Kwa amri ya Kristo, kwa njia yoyote kati ya mbili hizi yaani kwa sheria (Kut. 20:3) na kwa ufunuo, tunamwabudu Mungu (Ufu. 22:9).
3.1.1.2 Mlengwa katika Maombi
Mwanadamu hupaswa kumwomba Bwana Mungu (Zab.3 9:12; 54:2) ambaye anasikia. Lolote uliombalo katika maombi utpokea kama ukiwa na imani (Mat. 21:22). Mfano wa jinsi ya kuomba unapatikana katika Sala ya Bwana ambayo ni muongozo au mfano wa jinsi ya kuomba uliotolewa na Kristo (Lk.11:2-4).
Mhimili wa kwanza kabisa wa mteule au huduma ni maombi na huduma au kuhudumia neon (Mdo.6:4). Baraza la wazee limepewa wajibu wa kuratibu mkakati wa maombi wa watakatifu (Ufu. 5:8).
3.1.1.3 Maombi ya Binafsi na ya pamoja Kuwaombea Wengine
Maombi ya pamoja kwa moyo mmoja ni mfano kama walivyofanya mitume (Mdo. 1:14). Hii hufanyika kwa ushiriki wa kanisa lote (Mdo. 12:5).
Maombi sio kwa ajili ya Kanisa tu; bali pia ni kwa wale wenye bidii lakini hawajatiwa nuru na kujitia chini ya haki ya Mungu. Kwakuwa Kristo ndio mwisho (au mlengwa) wa sheria ambaye kila amwaminiye ahesabiwe haki (Rum 10:1-4).
Maombi huleta msaada. Mibaraka inayotokana na majibu ya maombi mengi, inafaa ishukuriwe pia kwa maombi mengi ya shukurani (2Kor. 1:11). Maombi lazima yawe katika roho (Efe.6:18). Lazima yawe maombi ya uvumilivu (Kol.4:2-4). Na hii ni silaha yenye kuwezesha kusimama imara katika kweli na utakatifu (Efe. 6:14).
Maombi ya mwenye haki yana nguvu katika kutenda kazi. Maombi yatokanayo na imani yanaweza kuponya mgonjwa na hutoa hakika ya msamaha wa dhambi. Kwahiyo tunaungamiana dhambi zetu sisi kwa sisi na kuombeana ili tupate kuponywa (Yak. 5:15-16).
3.2
Uhusiano kati ya Wokovu na Sheria
3.2.1 Mungu ndiye Mwamba Wetu
Mungu ndiye Mwamba wetu, nguvu zetu na wokovu wetu ambaye kwa yeye tunapata kimbilio letu (Zab.18:1-2). Kunamwamini yeye na hatuogopi (Isa. 12:2). Ufahamu kuhusu wokovu ni kazi ya Kristo na manabii (Lk. 1:77). Ufahamu huu limepewa Kanisa ambako watakatifu ni watumishi wa siri za Mungu (1Kor. 4:1). Wokovu unatoka kwa Wayahudi (4:22). Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine lolote chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokoleawa kwalo (Mdo. 4:12). Hivyo basi wokovu hupatikana kupitia Injili, kama ni uweza wa Mungu uletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia. Kwa njia ya Injili, haki ya Mungu inadhihirishwa kwa imani kwakuwa mwenye haki ataishi kwa imani (Rum.1:14-17). Mungu hakumkusudia mwanadamu akutane ha hasira, bali apate wokovu kupitia Yesu Kristo (1The. 5:9).
Kumwelewa Mungu husababisha mtu kujisikia sononeko la kimungu, ambayo huleta toka liletalo ondoleo la dhambi (2Kor. 7:10). Vivyo basi, Injili ni neno la kweli na ni pia ni Injili ya wokovu ambayo humfanya kila anayetubu apingwe muhuri na Roho Mtakatifu (Efe.1:13). Wokovu hupatikana kwa kuyaamini maandiko matakatifu. Kwa kuvuviwa na Mungu, Maandiko yaweza kumwelekeza mfanya toba kwenye wokovu kwa njia ya imani katika Yesu Kristo (2Tim. 3:15-16). Na, ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso yaliyo mpata; naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii; (Ebr. 5:8-9).
Kwahiyo alitolewa mara moja tu ili azichukue dhambi na atakuja tena mara ya pili, sio kuja kuchukua dhambi ila kuja kuwaokoa wale wote ambao walikuwa wanamngea kwa uaminifu na hamu (Ebr. 9:28). Kwahiyo Wokovu ni muhimu kwa wote na umetolewa mara moja tu kwa watakatifu (Yuda 3). Hivyo basi, hakuna tena ufunuo wa aina yoyote mpya ambao alipewa Yesu Kristo na Mungu na akampa Mtume Yohana. Chochote kile kinacho husu wokovu wa mwanadamu kimeandikwa katika Biblia. Wokovu, nguvu na utukufu ni vya Mungu na ame wafunulia watumishi wake kupitia Kristo na inatakiwa kushikilia visibadilike (Ufu.22:18-19).
Kutiwa muhuri kwa mara ya mwisho kwa watakatifu ni kupitia Roho Mtakatifu sawasawa na sheria za Mungu kama zilivyo funuliwa katika Biblia katika Agano la Kale vikithibitishwa na sheria.
Kristo alitoa sheria pale Sinai kama Malaika wa Agano au Uwepo wa Malaika wa Yahweh. Alisema kwamba:
…Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati havitaondoka, hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakaye vyunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. (Mat. 5:18-19).
Ndiyo maana Kristo kwa namna yoyote ile hakuvunja sheria. Alizishika sheria na aliwaamuru watu kufanya vivyohivyo. Torati na manabii vilikuwepo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu (au hujichomeka humo) (Lk.16:16).
Lakini ni vyepesi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati (Lk. 16:17).
Sheria ilitolewa na kupitia Musa, ila hazikushikwa (Yoh. 7:19). Wale watendao dhambi chini ya sheria, wataangamia chini ya sheria (Rum. 2:12) kwakuwa dhambi ni uasi au ni uvunjaji wa sheria (1Yoh.314). Tohara ni ya moyoni na ushikaji wa misingi ya sheria ni kipimo cha tohara hiyo. Yeye ashikaye sheria amesha pata tohara ya moyoni, na yule aliyetahiriwa kimwili lakini hazishiki sheria ni sawa na mgumu ambaye si mwaminifu. Wale walio Wayahudi ni wale wazishikao sheria tokea mioyoni mwao ni Wayahudi wa kiroho. Hivyo basi, wale wasemao kuwa ni Wayahudi, na kumbe sio, watahukumiwa Ufu.3:9) na watakuja jinyenyekesha kwa watakatifu. (Aina hii ya kunyenyekea inatafsiriwa pia kama kusujudu na itafanya kwa Kristo na watakatifu).
Torati ni takatifu na hizi amri ni takatifu na za haki na ni njema (Rum. 7:12). Kwahiyo, Torati haisababishi mauti lakini ni ile dhambi ambaya tafsiri yake ni uvunjaji wa sheria, inayofanya kazi ndani ya moyo wa mtu (Rum. 7:13).
Torati ni ya kiroho lakini mwanadamu ndio aliye ni wa kimwili, aliye uzwa katika utumwa wa dhambi (Rum.7:14). Mwongofu wa kweli ni lazima ataifurahia sheria ya Mungu moyoni mwake (Zab.119:1ff.; Rum.7:22). Kwakuwa sheria huwaongoza watu kaw Kristo ambaye ndiye mwisho wa sheria (Rum. 10:4). Kuongozwa na Roho humuweka mtu huru na sheria (Gal. 5:18). Siyo kuwa Roho huiondoa ile sheria, la hasha bali hutuwezesha kishika ile sheria kirahisi toka moyoni na kwa matendo mema katika asili yetu (Ebr. 8:10-13). Sheria za Mungu hufuatwa kwa njia ya imani na sio kwa kazi au matendo (Rum. 9:32). Kuzitii sheria ni kitu muhium katika kumpendeza Roho Mtakatifu akaaye ndani yao wazishikao Amri za Mungu (1Yoh.3:24; Mdo.5:32). Kwahiyo, haiwezekani kuwa Mkristo na kumpenda na Kristo bila kushika sheria za Torati. Hii ni muhimu, ikijumlisha na ushikaji wa Sabato kama ni amri ya nne.
3.2.2
Wokovu Kwa Neema
Maana neema ya Mungu iwaokowayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tama za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; tukilitazama tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; (Tit. 2:11-13, soma Biblia iitwayo Marshall’s RSV Interlinear Greek-English New Testament). Kwahiyo Kristo ni mwonekano wa utukufu wa Mungu Mkuu ambaye ni Mwokozi wetu (Tit. 2:10). Kwahiyo, neema ni matokeo ya kazi ya Yesu Kristo.
Kanisa linalindwa kwa nguvu za Mungu kwa njia ya imani kwa wokovu utakao funuliwa katika siku za mwisho (1Pet. 1:5). Matokeo ya imani ni wokovu wa roho. Manabii walitabiri kuhusu wokovu lakini hawakujua majira wala mtu huyu Masihi wakati wakitabiri mateso yake na ukuu wa ukufu wake (1Pet.1:9-10).
Dhambi ziliingia duniani kupitia Adamu na zilitawala kuanzia Adamu hadi Musa. Mauti ilikuwa ndio matokeo ya dhambi (Rum. 5:12). Dhambi ilikuwepo kabla Torati haijatolewa kwa Musa (Rum.5:13). Kwahiyo, matokeo ya Torati yalikwisha fahamika tayari tokea Adamu, kuwa dhambi hazihesabiwi pasipo sheria. Kwahiyo, neema imetolewa kwa wingi kwa sababu ya kumkomboa mwanadamu na dhambi na sheria. Wakati dhambi zilivyokuwa nyingi, chini ya sheria, neema ilikuwa nyingi (Rum. 5:15-21). Kwa kutii kwake mtu mmoja wengi wamewezeshwa kupata haki kwa neema itokanayo na haki hadi uzima wa milele katika Yesu mpakwa mafuta. (Rum. 5:20-21). Sasa basi, hakuna hukumu ya dhambi juu yao walio katika Kristo Yesu (Rum. 8:1). Kwahiyo, sheria imetimilika kwetu sisi tunao enenda katika Roho (Rum. 8:4).
Roho huongoza nia zetu ili ziyafanye mapenzi yake (Rum. 8:5). Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu wala haiwezi kuitii (Rum. 8:7). Hivyo basi, mawazo ya kimwili au ya mtu asiye ongoka hujulikana pale yanapo shindana katika kukubaliana na kuzishika sheria za Mungu.
Lakini, ikiwa Roho wake yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu (Rum. 8:11). Kwakuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu (Rum. 8:14) nah ii ni kwa neema ya Mungu. Kwakuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo (Yoh. 1:17). Kwahiyo twalia Aba, yaani Baba, kuendeleza hali hii ya uwana (Rum. 8:15) kama ilivyotolewa kwa kaka yetu Yesu Kristo.
Torati yenywe peke yake haitoi haki. Mtu huhesabiwa haki kwa njia ya imani katika Yesu Kristo (Gal. 2:16). Maisha wanayoishi ni kwa imani kupitia Mwana wa Mungu (Gal. 2:20). Maana mimi kwa njia ya sheria nalifia sheria ili nimwishie Mungu (Gal. 2:19). Siibatili neema ya Mungu; maana, ikiwa haki hupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure (Gal. 2:21). Tunashika sheria kwasababu Roho hutuongoza na sheria hutangulia mbele ya ili asili ya Mungu ambayo ambayo tumewekwa ndani yake na sisi tukiwa ni warithi (2Pet. 1:4) kama ilivyo kwa Kristo.
Tumeokolewa sio kwa sheria bali ni kwa neema ya Yesu Kristo (Mdo.15:11). Dhambi haziwatawali wateule kwasababu hawapo chini ya sheria bali chini ya neema na wamejitia chini ya haki ya Mungu (Rum.6:14-15). Walakini, hatufanyi dhambi kwa kuvunja sheria kwa sababu sisi ni watumwa wa Mungu na haki na sio watumwa wa dhambi, tukitii kutoka mioyoni mwetu sawa na kiwango cha mafundisho ambayo tumejitoa kwayo (Rum. 6:17-18). Hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, mmeokolewa kwa neema (Efe. 2:5). Ametufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu waroho, katika Kristo Yesu; ili katika zamani zinazo kuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi kwa neema yake kwetu sisi katika Kristo Yesu (Efe.2:6-7). Wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu (Efe.2:9). Kwahiyo, tunashika sheria kwa Roho wa Mungu kwa neema.
3.2.3
Ulazima wa kuwa Chini ya Sheria
Kuna ulazima usio na mwisho wa kuishika sheria, wa kudumu milele kama ilivyoandikwa (Mat. 3:18; Lk.16:17). Haikuwa inashikwa sawasawa na Wayahudi wakati ule wa Kristo (Yoh.7:19), ilikuwa imechanganywa na mapokeo (Mat.15:2-3,6; Mk.7:3,5,8-9,13). Waalimu wa Kiyahudi wa zama zile waliwatwisha mizigo na kongwa ikawafikisha mahali pa kumjaribu Mungu (Mdo.15:10).Kuna amri au agizo kutoka juu ya kushika amri za Mungu. Zinadumu na kamwe hazitapita mpaka ukamilifu wa dahari wa kuwepo kwa mwanadamu.
3.2.3.1 Kwanini Wakristo Washike
Sheria
Wakristo wameokolewa kwa neema na sio kwa sheria. Kwa nini basi ionakane kuwa ni muhimu kushika sheria? Ni kulingana na sababu zifuatazo:
Sheria za Mungu ziliwekwa kulingana na asili ya wema wake.
Sheria za Mungu inatokana na asili yake Mungu na hivyo basi inasimama milele kwakuwa Mungu mwenyewe habadiliki, akiwa ni mwema sana akiwa ni kituo cha wema na upedo. Katika Marko 10:18, Kristo alisema: kwanini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu au kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri (Mat.19:17). Asili ya Mungu ni wema usio badilika. Jeshi la mbinguni limerithi asili yake hii ya kimbinguni. Wanafanyika wakati wote kuwa katika asili hii ya kimbinguni ambayo ni ya wema.
Kwa jinsi hiyo, Kristo ni yeye yule habadiliki jana, leo na katika zama zote (aioonas) (Ebr.13:8). Wateule, katika kurithi kuhu asili ya kimbinguni (Pet. 1:4), hufanyika kuwa ni sehemu ya ukuhani wa kimbinguni, ule wa Melkizedeki ambao hudumu milele na haubadiliki (oparabaton) au haubadiliki kizazi hadi kizazi (aioona) (Ebr. 7:24). Kristo aweza kuwaokoa wote wamnjiao Mungu kupitia yeye (soma, Ebr. 7:25 katika Marshall’s Greek-English Interlinear) Lakini yeye sio mlengwa katika kuabudu wala Mungu hajaamuru kufanyika jambo namna hiyo kuwa ni mapenzi yake.
Sheria ya Mungu ni ya kuifuata kwa imani na sio kwa kazi (Rum. 9:32). Tunalo Agano Jipya ambalo Bwana ameweka sheria zake ndani ya mawazo yetu na kuziandika mioyoni mwetu. Yeye ni Mungu nasi ni watumishi wake, tumuabuduye kwa kuzishika sheria zake katika hali yetu ya asili (Ebr. 8:10-13). Kwahiyo, hakuna ishara nyingine ya nje ila ni kwa kuzishika amri za Mungu kati yetu ambazo ndio tohara yetu (1Kor. 7:19) kama Wakristo na washirika wa Israeli ya kiroho. Ni wale wanao mkasirisha joka kwa kuzishika amri za Mungu. Ushikaji wa amri za Mungu huwatambulisha katika kipindi cha mateso (Ufu.12:17). Hawa ndio watakatifu wazishikao amri za Mungu na subira (Ufu. 14:12).
3.2.3.2 Wakristo
kama Hekalu la Mungu
Watakatifu ni Hekalu au
Sinagogi naos, la Mungu na Roho wa
Mungu anakaa ndani yake. Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu
mtu huyo. Kwa maana Hekalu la Mungu ni takatifu ambalo ndilo ninyi
(1Kor.31617). Kwa ajili hiyo kuna ulazima kwa Wakristo kutunza miili yao kiafya
kama apendavyo Roho wa Mungu kwakuwa Mungu alisema yeye atakaa ndani yetu na
kutembea pamoja nasinaye atakuwa Mungu wetu. Tunapaswa kuishi katika utakatifu
na kujitenga na mambo ya ulimwengu huu. Mungu awe ni Baba yetu na sisi tuwe
watoto wake (2Kor. 6:16-18 sehemu nyingi imenuu aya za Agano la Kale, Walawi
26:12; Eze.37:27; Isa.52:11; 2Sam.7:14).
Kwa ajili hiyo, Wakristo
wanatakiwa wasifungiwe nira pamoja na wasioamini kwa jinsi isivyo sawasawa
(2Kor. 6:14). Yawapasa kajitakasa na kila aina ya unajisi wa mwili na roho, ili
kutunza kikamilifu utakatifu katika kicho cha Mungu (2Kor.7:1). Kwahiyo
wamechaguliwa tangia mwanzo na kuokolewa kwa njia ya utakaso na Roho kwa
kuiamini kweli (2The. 2:14). Kuiamini kweli ni muhimu katika kupata afya ya
akili na ni alama kwa wateule. Inaonekana wazi kuwa Biblia na amri zilizoko
ndani yake zina umuhimu na malengo katika maisha. Upimaji wa Hekalu la Mungu
hufanyika kupitia sheria hizi (Ufu.11:1).
3.2.4 Amri
Kumi Za Mungu
Kanisa linatakiwa kuzishika amri kumi za Mungu kama zilivyo elekezwa
katika Kutoka 20:1-17 na Kumbukumbu la Torati 5:6-21.
Amri ya kwanza inasema:
Mimi
ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya
utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Mungu Baba ni Mungu wa pekee
wa kweli (Yoh.17:3) na hakuna elohim mwingine kuwepo kabla yake, au aliye sawa
naye. Kwakweli hairuhusiwi kukiabidu au kuonba kiumbe kingine chochote akiwemo
Yesu Kristo.
Amri ya Pili inasema:
Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu
chochote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini
chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia; kwakuwa mimi, BWANA, Mungu waku
ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu
na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na
kuzishika amri zangu.
Kwahiyo basi, tunaona kwamba hairuhusiwi kujifanyia sanamu ya kuchonga au mfano wa kitu wa kitu chochote kwa matumizi yoyote yale, iwe ni ibada za kidini au kwa ajiliya nembo ya kidini. Hii inamaanisha pia kuwa hata msalaba ni miongoni mwa vitu vilivyo katazwa kutumiwa kama nembo ya Kanisa.
Hizi amri zenyewe tu
zinaunda utambulisho wa mfumo wa kidini na zote zinazungushiwa hivyo.
Amri ya Tatu inasema:
Usilitaje
bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu
alitajaye jina lake bure.
Jina la Bwana Mungu lina
mamlaka na kwahiyo amri hii sio tu kuwa inashughulika na namna tu ya makufuru,
bali inafikia hata kwenye hatua ya kuhusikana na matimizi mabaya ya mamlaka ya
Kanisa na wale wote wanaoenenda vibaya tofauti na maelekezo ya Mungu kupitia
Yesu Kristo.
Amri ya Nne inasema:
Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwahiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
Sabato ya kila siku ya saba
ya juma, ni ya muhimu sana kwa wokovu na imani yetu. Hakuna Mkristo anayedai
kuwa anamuishia Mungu na huku akishindwa na kudharau kuishika Sabato, ambayo
kwa kalenda za leo inaangukia siku ya Jumamosi. Tendo la kuanzilisha siku
nyingine na kuifanya kuwa ni ya ibada tofauti na ile ya siku ya saba ya juma
sio tu kuwa inaitia unajisi bali inakuwa ni miongoni ya ibada ya sanamu ambayo
ni chukizo na ni kuyaasi mapenzi ya Mungu. Ni tendo la uasi ambao umefananishwa
na dhambi ya uchawi (1Sam.15:23). Ikiunganishwa na amri ya pili ambayo
inaongelea kuhusu kumuabudu Mungu peke yake hivyo kukiuka amri ya nne ni ibada
ya sanamu. Tendo la kutunga kalenda nyingine ambayo inaiyumbisha kalenda halisi
ya wiki kwa kuongeza siku moja mbele katika mzunguko halisi kuna endeleza maana
ileile.
Amri hizi nne za mwanzo
zinahusu mahusiano kati ya mwanadamu na Mungu na zinajulikana kama ni kundi la
amri ya kwanza iliyo kuu isemayo kuwa: Nawe pende Bwana Mungu wako
kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na
kwa akili zako zote, (na kwa nguvu zako zote Mk 12:30). Hii
ndio amri iliyokuu tena ni ya kwanza (Mat. 22:37-38).
Njia pekee ya kujionyesha
kuwa mtu kuwa anamjua na kumtii Mungu ni kwa kuzishika hizi amri, na kuangalia
kutozivunja.
Amri kuu ya pili ni:
Mpende
jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi (Mat.22:39; Mk.12:31).
Amri kuu ya pili inahusu uhusiano uliotajwa katika amri zile sita za mwisho kati ya kumi ambazo zinahusu mahusiano kati ya wanadamu.
Amri ya tano inasema:
Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.
Uhusiano katika familia ni tofali la muhimu katika ujenzi wa msingi katika jamii na inaashiria msimamo wa kimaadili wa jinsi dini ilivyo mahali popote pale duniani.
Amri ya Sita inasema:
Usiue
Hukumu imewekwa juu ya Wakristo wenye kuvunja amri inayosema usimuonee hasira ndugu yako. Kuwaka hasira ni kufanya fujo au kugombana na jirani yako. Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanam ya moto (au kaburi au kuzimu) (Mat.5:22)
Amri ya Saba inasema:
Hukumu imewekwa juu ya Wakristo wenye kuvunja amri inayosema usiwakiane tamaa na mtu mwingine ambaye sio mwenzi wako wa ndoa (Mat.5:28).
Amri ya Nane inasema:
Kuiba ni kutenda kosa kwa jirani yako, jambo linalo pelekea wewe kujunja uhusiano wako na Mungu.
Amri ya Tisa inasema:
Utakatifu na haki ni maneno kwakweli yaliyochua maana moja tu katika lugha ya Kiebrania. Inamaana kuwa Kristo hawezi kuwa mtakatifu bila kuwa ni mtu wa haki. Hali ya kugeuza haki kwa kutoa ushahidi wa uongo kunaathirivi maisha ya wokovu wa Mkristo.
Amri ya Kumi inasema:
Usitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa
jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda
wake, wala chochote alichonacho jirani yako.
Tamaa ni hatua inayo wapelekea watu hatimaye kuiba vitu au kufanya mahusiano ya kiuasherati na kuathiri uhusiano na Mungu. Kwa minjiri hii hii inakuwa ni ibada ya sanamu. Inafanya kiwepo kitu kingine cha kukilenga katika kutimiliza haja zako huku ikienda kinyume na zile amri nyingine. Kwa mtazamo huu utaona kuwa amri hizi zinaenda kwa mzunguko unao tegemeana na hivyo uhusiano wa tamaa unakuwa ni chanzo cha kuvunja zile nyingine, na hivyo uvunjaji wa amri moja tu kati ya hizi, humaanisha kuwa umevunja nyingine zote pia. Kwahiyo hakuna ruhusa yoyote kuhusisha na dhambi. Dhambi ni uasi au uvunjaji wa sheria. Kristo alifundisha jinsi unavyoweza kufahamu sheria kiukweli katika Mathayo 5:21-48; zikihusiana na Kutoka 20:13; Kumbukumbu la Torati 5:17, 16:18 na vilevile Luka 12:57-59.
Amri hizi zinapaswa wazazi
wawafundishwe watoto wao kwa bidii, kadiri watoto wanavyokua. Yawe dalili juu
ya mikono na kama utepe ktikati ya macho yako (kwa nadharia na matendo) na
yaandikwe juu ya miimo ya nyumba (Kum.6:7-9).
3.2.5 Sheria nyingine zitawalazo Mwenendo wa Mwanadamu
3.2.5.1 Shera ya Vyakula