Makanisa Ya Kikristo ya Mungu
[122]
Migawanyo Mikuu ya Makanisa Yanayoishika—Sabato
(Toleo la 2.1 19950624-19991205)
Jarida hli muhimu linaelezea kwa kufuatilia Makanisa Yanayoitunza—Sabato kuanzia kwenye karne ya kwanza katika Mashariki ya Kati, Ulaya na kwa bara Asia yote. Ikifunika mhimili wa kipindi cha Milenia mbili ni rekodi inayofahamika sio tu kwa Makanisa bali pia ni kwa marefu ambayo mfumo wa kuabudu siku ya Jumapili umefikilia kufuta mfumo wa ibada za Sabato kwa kutumia utesaji wanaoamini hivyo.
Christian Churches of God
PO Box 369, WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
E-mail: secretary@ccg.org
(Copyright © 1995, 1998, 1999 Wade Cox)
Masomo haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org and http://www.ccg.org
Migawanyo Mikuu ya Makanisa Yanayoishika—Sabato
Historia yake
Kutokana na mahojiano ya historia ya Makanisa Yanayoishika—Sabato, tunaweza kupata maadhi ya hitimisho muhimu kuhusiana na wakati na pia kufuatilia mfumo au utaratibu wa utii, unaoonyesha jinsi utaratibu wa kibiblia kama ulivyoanzishwa na Kristo, kuwa kamwe haukukoma. Kuna idadi kubwa ya mifano inayoashiria konyesha kuwa mfuatano wa kihistoria wa kuwepo kwa mnyororo wa Makanisa yanayoitunza—Sabato kwa wakati wote wa kuanzia kipindi cha ulimwengu wa Wakristo wa Kwanza na huko Ulaya, kabla na baada ya kipindi kijulikanacho kama Zama za Kati. Haya yote yanaendelea mbele zaidi, na kupitia, Matengenezo. Makanisa yanayoishika—Sabato, pia yanaitwa Sabbatati, yameendelea kudumu kwa hatua au kipindi kimoja au nyjngine kubwa zaidi ya sehemu ya dunia. Makanisa haya pia yanaonekana kuwa katika kiini chake cha kati, kutoka kiini chao cha kati, kutoka kwenye hatua ya kati, zilitunza Siku Takatifu.
Maadhimisho ya Sabato yalienea kutekote na inaonekana kupingwa kutoka Roma. Sabato na hizi Siku Takatifu ziliadhimishwa huko Misri kama maandiko ya kwenye Magombo ya Oxyrhynchus (ya takriban miaka ya 200-250 BK) yanavyoonyesha kusema:
Iwapo kama hamtaifanya Sabato kuwa ni Sabato ya kweli [Yaani kuitakatifuza Sabato], hamtamuona Baba (kwa mujibu wa magombo yajulikanayo kama the Oxyrhynchus Papyri,. Pt. 1, p. 3, Logion 2, verso 4-11, London: offices of the Egyptian Exploration Fund 1898).
Origen pia aliwaunganisha washika—Sabato akisema:
Baada ya sikukuu ya ongezeko la dhabihu [kusulibiwa] zimefanywa maadhimisho ya pili ya Sabato, na inakubalika kwa ye yote aliye mwenye haki miongoni mwa watakatifu pia washike maadhimisho ya sikukuu ya Sabato. Inabaki pale kwahiyo sabbatismus, ambayo, utunzaji wa Sabato, kwa watu wa Mungu [Waebrania 4:9] (Hotuba ya Hesabu 23, kifungu cha 4, kwenye Migne, Patrlogia Graeca, Vol. 12, cols. 749, 750).
Sawa na kama ilivyo kwenye Katiba ya Mitume Watakatifu (Ante-Nicene Fathers, Vol. 7, p. 413; c. 3rd centuary) inavyosema:
Nanyi mtaitunza Sabato, kwa utukufu wa yeye aliyeacha kufanya kazi ya uumbaji, lakini lakini sio kwa kazi yake ya utoaji wa ridhiki: ni mapumziko ya kuzitafakari sheria, na sio kwa ajili ya uzembe au uvivu wa kuishi mikono mitupu.
Washika—Sabato, sehemu asilia ya Kanisa, lilienea maeneo ya magharibi hadi kufikia Ulaya na kutoka Palestina, likaenea hadi kufika Mashariki mwa India [kwa mujibu wa jarida la Mingana kuhusu Ueneaji wa Kwanza wa Ukristo, yaani (Early Spread of Christianity, Vol. 10, p. 460)] na kisha hadi Uchina. Utambulisho wa washika—Sabato nchini India kulisababisha utata kwenye imani ya Buddha kunako mwaka 220 BK. kwa mujibu wa Lloyd (kitabu chake cha Fundisho la Ukiri wa Imani wa Nusu ya Wajapani, yaani The Creed of Half Japan, p. 23), Kizazi cha Ufalme cha Kushan cha Kaskazini mwa India, kiliitisha baraza la makuhani wa Kibuddha huko vaisalia, ili kuleta usawa miongini mwa watawa wa Kibuddha kwa ajili ya maadhimisho yao ya Sabato ya kila juma. Baadhi yao walivutiwa sana na maandiko ya Agano la Kale na kuwa walikuwa wameanza tayari kuitunza Sabato.
Wasabbatati wa Ulaya walikuwa hawachukuliwi katika kulazimishwa. Kanisa lililoanzishwa huko Milani liliitunza Sabato.
Lilikuwa ni tendo la jumla kwa Makanisa ya Mashariki, na kwa baadhi ya Makanisa ya pande za Magharibi…. Kwa kuwa katika Kanisa la Millaine [Milani], ….inaonekana kuwa siku ya Jumamosi ilifanywa kuwa ni siku ya maadhimisho matakatifu yaani farre esteeme…. Sio kwamba Makanisa ya pande za Mashariki, au pande ye yote iliyobakia ambayo iliadhimisha siku ile kuwa walihusika na lundaisme [imani ya Kiyahudi]; lakini kwamba walifanyika kwa pamoja kwa siku ya Sabato, ili kumuabudu Iesus [Yesu] Kristo Bwana wa Sabato (jarida la Dkt. Peter heylyn kisemacho Historia ya Sabato, yaani History of Sabbath, London 1636, Part 2, para 5, pp. 73-74; speling ya asilia imeazimwa).
Makanisa ya magharibi yakiwa chini ya Wagothiki, wenyewe hawakuwa wakatoliki, lakini ni Waaminifu wa kile kilichokuwa kinaitwa mafundisho ya Waariani. Sidonius anasema kwamba chini ya theodoric mnamo kwenye miaka ya 454-526 kwamba:
Ni ukweli kwamba ilikuwa ni desturi ya watu wa Mashariki kuitunza Sabato kwa jinsi ile ile kama ni siku ya Bwana na kuitisha makusanyiko matakatifu wakati kwa upande mwingine, watu wa pande za Magharibi, wanaoishindania siku ya Bwana wakiacha kushika maadhimisho ya Sabato (soma jarida la Apollinaris Sidonii Epistolae, lib. 1.2; Migne, 57; yaani Waraka wa Apollinaris).
Hata hivyo, Wagothiki wa pande za Magharibi, walioondoka kwenda pande za Kusini ya Gaul na Hispania, walikuwa ni washika kasumba na waliitwa ni Wanosiani walioaminika kuwa walitokea Bonosus ya Sardica, waliofundisha kuwa Yusufu na Mariamu walikuwa na watoto. Aliwekwa kwenye hali moja na Marcellus na Photius, na hivyo kuashiria kwamba walikuwa na nia sawa wakiiona Sabato na sheria.
Hii inaonekana pia kusaidiwa na ukweli kwamba Marseilles ilikuwa ni makao makuu ya wale waliojulikana tangu mwanzo wa pande za Magharibi (massilians), ambao waliofika kwa vingi pale na hatimaye wakatuhumiwa kama wa imani ya Upelagiani (huenda kimakosa) huko mjini Orange mnamo mwaka 529 (tazama jarida la ERE, Sect, Vol. XI. P. 319).
Kutokana na kanuni ya 26 ya Baraza la Elvira (takriban mwaka 305), inaonekana kwamba Kanisa katika Uhispania liliitunza Sabato. Rumi walianzisha tendo la kufunga saumu siku ya Sabato ili kuzuia au kuharibu nguvu za wale wanaoitunza—Sabato. Papa Sylvester (miaka ya 314-335) alikuwa ni wa kwanza kuyaamuru Makanisa kufunga saumu siku ya Sabato ili kupingana nayo, na Papa Innocent (miaka ya 402-417) alilifanya jambo hili kuwa ni amri ya muhimu ifanyike Makanisani kwa kuheshimu yeye.
Innocent aliamuru kuwa siku za Jumamosi au siku za Sabato ziwe siku za kufunga saumu kila zinapofika (kwa kujibu wa Peter Heylyn, jarida la Historia ya Sabato yaani History of Sabbath, Part 2, Ch. 2, London, 1636, p. 44).
Kanuni ya 26 ya Baraza la Elvira linasema:
Kama kufunga kila siku ya Sabato: Kulikusudiwa, kwenye kosa lile lirekebishwe kwa kufunga kila siku ya Sabato.
Mji wa Sabadelli ulioko Kaskazini-Mashariki ya Hispania karibu na jiji la Barcelona ukiitwa jina lake kwa ajili ya Washika Sabato yaani Wasabbatati au Wavaldeases (au Wavallenses). Umri wa jina na zama zake kwa majina ya Sabbatati au insabbatati, yalionyesha kuwa kinyume na hali ya Waldo kuanzisha kwake imani ya Wavallense, lakini zaidi sana ni mgawanyo wao huonyesha kwamba alikuwa ni mwongofu na wao, na akachukua jina lake kutoka kwao kama wataona.
Makanisa ya watunza—Sabato katika pande za Umedi yaani Persia yaliendelea na miaka arobaini ya mateso chini ya Shapur II, kipindi cha miaka ya 335-375 rasmi, kwa sababu tu ya kwamba wao walikuwa ni watunza—Sabato.
Wanamdhalilisha na kumdharau mungu-jua wetu. Hakuwa Zoroaster, aliyefanyika kuwa mtakatifu mwanzilishi wa imani ya kimbinguni, akaanzisha Jumapili miaka elfu moja iliyopita kwa heshima ya jua na kuipandikiza Sabato ya Agano la Kale. Tena hawa Wakristo wana ibada ya kimungu ya Jumamosi (kwa mujibu wa jarida la O’Leary la Kanisa la Kisyria na Mababa, yaani, The Syriac Church and Fathers, pp. 83-84, ambalo limenukuu jarida la Kweli Ishindayo, yaani Truth Triumphant p. 170).
Maseso haya yalilenga pande za Magharibi na Baraza la Laodikia (takriban mwaka 366). Hefele anaandika kuwa:
Kanuni ya 16 inasema – Injili kwa pamoja na Maandiko Matakatifu mengine visomwe siku za Sabato (sawa na zisemavyo pia kanuni za 49 na 51, jarida la Bacchiocchi, fn. 15, p. 217).
Kanuni ya 29 inasema – Wakristo hawapaswi kujifananisha na Wayahudi kwa kufanya mapumziko siku ya Sabato, lakini lazima wafanye kazi siku ile ili kuipa heshima zaidi siku ya Bwana ya kwa kupumzika, kama ikiwezekana, kama Wakristo. Hata hivyo iwapo kama kuna mtu atakutwa akijitia kwenye kasumba ya kiyahudi, basi na walaaniwe na kuondolewa kwenye Ukristo (mansi, II, pp. 569-570, tazama Hefele Councils, Vol. 2, b.6).
Mwanahistoria aitwaye Socrates anasema:
Kwa kupitia karibu Makanisa yote dunia inaadhimisha fumbo takatifu [linalodhaniwa na Wakatoliki kuwa ni ekaristi au Ushirika wa Meza ya Bwana kama wanavyouita] siku ya Sabato ya kila wiki, ila Wakristo wa Alexandria na Rumi, wakiitunza kwenye siku ile ile iliyokuwepo kwa kufuata mapokeo ya zamani, walikataa kufanya hii (Socrates, Ecclesiastical History, yaani Historia ya Kanisa, Kitabu cha. 5, sura ya 22, ukurasa wa 289).
Sabato ilikuwa inatunza pia kwenye karne ya tano na Wakristo (Lyman Coleman jarida la Namna Ukristo wa Kale Ulivyokuwa yaani Ancient Christianity Exemplified, Sura ya 26, Kifungu cha 2, ukurasa wa 527). Kwa hakika, kama ilivyokuwa siku za Jerome (mwaka 420), Wakristo waliojitoa na kuwa waaminifu walifanya kazi za kawaida siku ya Jumapili (kwa mujibu wa Dkt. White, askofu wa Ely, kwenye jarida lake la Kuifanyia vitisho Siku ya Sabato, uk. 219).
Augustine wa Hippo, mshika Jumapili aliyejitoa sana kwa ibada hizi, alijaribu na kuona kuwa Sabato ilikuwa inaadhimishwa kwa sehemu kuu ya ulimwengu wa Wakristo [kwa mujibu wa jarida la Mababa wa Wakati wa Nikea na Baada ya—Nikea yaani Nicene and Post-Nicene Fathers (NPNF), Vol. 1, pp. 353-354)] na kuujutia ukweli kwamba kwenye Makanisa mawili jirani ya Afrika, moja lilikuwa linaadhimisha Sabato ya siku ya saba ya juma, wakati huo huo jingine likiwa linafunga saumu ili kuikomesha isiendelee (jarida la Peter Heylyn, op. cit, p. 416).
Makanisa katika ujumla wake yaliitunza Sabato kwa wakati fulani.
Wakristo wa zamani walikuwa makini sana katika kuiadhmisha siku ya Jumamosi, au siku ya saba ya juma…. Ni mpango kuwa makanisa ya pande Mashariki, na sehemu kubwa sana ya dunia, waliiadhimisha Sabato kama siku ya maadhimisho…. Athanasius vilevile aanatuambia waliitisha makutaniko ya kidini siku ya Sabato, sio ni kwa sababu walikuwa wameathirika na dini ya Kiyahudi, lakini kumuabudu Yesu, aliye Bwana wa Sabato, Epiphanius abasema vivo hivyo (kwa mujibu wa jarida la Zamani za Kanisa la Kikristo, yaani, Antiquities of Christian Church, Vol. II, Bk. xx, Ch. 3, Sehemu ya I, 66. 1137, 1136).
Katika kipindi cha nusu ya karne ya nne, askofu wa Kanisa linalotunza-Sabato la Waabyssia (Wahabeshi), Museus, alitembelea Uchina. Ambose wa alisema kwamba Museus alisafiri karibu kila mahali katika nchi ya Seres (Uchina), (kwa mujibu wa jarida la Ambrose, la De Moribus, brachman-orium Opera Omnia, 1132, lililokutwa huko Migne, Patriologia Latina, Vol. 17, kurasa za 1131-1132). Mingana anashikilia kuamini kwamba Waabyssinia Museus alisafiri hadi Uarabuni, Uajemi, India na Uchina mwaka 370 (tazama pia jarida la fn. 27 Kweli Ishindayo, yaani Truth Triumphant, p. 308).
Makanisa ya Kisabato yalianzishwa huko Uajemi na katikati ya ukingo wa mto Tigri na Frati. Waliitunza Sabato na kutoa zaka makanisani mwao (kwa mujibu wa kitabu cha maarifa kiitwacho Realencyclopaeie fur Protestantishe und Kirche, art. Nestorianer, tazama pia jarida la Yule liitwalo Kitabu cha Bwana Marco Polo, maarufu kama The Book of Ser Marco Polo, Vol. 2, p. 409). Wakristo wa Mtakatifu Thomasi wa India kamwe hawakuwa na mahusiano na Rumi.
Walikuwa ni watunza-Sabato, kama walivyokuwa hao waliovunja kabisa mahusiano na Rumi baada ya Baraza la Chalcedon (Kalkedoni), walioitwa Waabyssia au Wahabeshi, Wayakobo, Wamaroni, na Waarmenia na Wakurdi, waliozitunza sheria za vyakula na kukataa mafundisho ya kuungama na ya toharani (kwa mujibu wa kitabu cha maarifa kilicho andikwa na Schaff-Herzog kiitwacho Kitabu Kipya cha Maarifa ya Elimu ya Kidini, yaani The New Encyclopaedia of Religeous Knowledge, art. Nesorianer aliye andikwa hapo juu).
Mnamo mwaka 781 Mnara maarufu wa nchini Uchina uliandikwa michoro ya kuelezea jinsi ukuaji wa imani ya Kikristo ilivyo nchini Uchina ilivyokuwa kwa wakati ule. Uandishi huo wa orodha ya maneno takriban 763 uligunduliwa baada ya kuchimbua eneo la mji wa Changan mnamo mwaka 1625 na inaaminika kuwa sasa mnara huu umesimamishwa kwenye Pori la Maandiko ya kale la Changan. Nakili za maandiko hayo zinasema hivi:
Katika siku ya saba tunatoa dhabihu, baada ya kuitakasa mioyo yetu, na kupata utakaso kwa ajili ya dhambi zetu. Dini hii, ni kamilifu sana na ni njema sana, ni vigumu kuitaja, lakini huliondoa giza kwa nuru ya mafundisho yake (jarida la M. l’Abbe Hue la Ukristo katika Uchina au Christianity in China, Toleo la 1, Sura ya 2, kurasa za 48-49).
Wayakobo wanatajwa kuwa walikuwa ni washika-Sabato wa nchini India mwaka 1625 jarida la Mahujaji au Pilgrimmes, Pt. 2, p. 1269)
Kanisa la Waabyssinia lilibakia likiishika-Sabato na nchini Ethiopia (Uhabeshi) Wajesuiti walijaribu kuwashawishi Waabyssia (Wahabeshi) waingie na kuukubali Ukatoliki. Waabyssia au Wahabeshi walipopelekwa kwenye mahakama ya Lisboni, wakakana kuwa walikuwa hawaishiki Sabato sio kwa sababu ya kuiga kasumba ya Wayahudi, bali ilikuwa ni kwa ajili ya kumtii Kristo na Mitume wake (jarida la Geddes la Historia ya Kanisa la Uhabeshi au Ethiopia, au Church History of Ethiopia, kurasa za 87-88). Wajesuit walimshawishi mfalme Zedenghel aamue kujisalimisha kwa Papa mnamo mwaka 1604, na kupiga marufuku utunzaji wa ibada za Kisabato kwa kuweka adhabu kali sana (jarida la Geddes, kama lisemavyo hapo juu ukurasa wa 311 na pia jarida la Gibbons la Kudhoofika na Kuanguka kwa Dola ya Rumi, Sura ya 47).
Sabato katika Utaliano au Italia
Inaaminika sana kuwa wafuasi wa Ambose wa Milan waliitunza Sabato huko Milan na waliokuweko Roma waliabudu siku ya Jumapili, na hivyo ndivyo ikawa chanzo cha usemi huu usemao kuwa Unapokuwa uko Rumi fanya kama wanavyofanya Warumi wenyewe (jarida la Heylyn, op. cit, 1612). Heylyn analifananisha Kanisa la Milan kuwa kutoka karne ya nne, kama kitovu au mhimili wa utunzaji wa Sabato kwa upande wa Magharibi (jarida hilo hilo lililotajwa hapo juu, sehemu ya 2, kifungu cha 5, kurasa za 73-74). Kwa hiyo sio jambo la kushangaza Wasabato au Wasabbatati walikuwa na shule yao kule, kama ilivyonukuliwa na Wavallensi kwa wakati ule ambao Peter Waldo alijiunga nao. Sabato ilikuwa inaadhimishwa nchini Utaliano kwa kipindi cha karne kadhaa na Baraza la Friaul (takriban mwaka 791) ndipo ikaongelewa na walei kwenye mwongozo au kanuni ya 13.
Tunawaamuru Wakristo wote kuabudu katika siku ya Bwana na kukutanika na sio kuipa heshima siku iliyopita ya Sabato, lakini kuupa umuhimu usiku ule mtakatifu ya siku ya kwanza ya juma inayoitwa siku ya kwanza ya Bwana. Unapokuwa unaiongelea Sabato ambayo Wayahudi huiadhimisha, siku ya mwisho ya juma na ambayo walei wetu huitunza…(Mansi, 13,85).
Kwa hiyo kulikuwa na vikundi vilivyokuwa vinashikilia mapokeo ya kuishika-Sabato huko Ulaya kati ya miji ya Milan na Lyons, ambako kulikuwa ni kitovu cha Watu Masikini wa Lyons, ambalo ni tawi la Wasabbatati au Wainsabatati, kama walivyokuwa wakiitwa, ambao baadae waliitwa Wawalensia. Muunganiko wa Milan na Lyon ulipata nguvu na Pothinus na Irenaeus (takriban mwaka 125-203). Wote wawili walikuwa ni wafuasi wa Polycarp, mwanafunzi wa Yohana yaani John na wote walikuwa ni watunza-Sabato. Irenaeus alifanyika kuwa ni askofu wa Lyons baada ya kuuliwa kwa Ponthinus mwaka 177 chini ya amri ya mateso ya Marcus Aurelius. Kanisa katika Lyons na Vienne, lilitaarifu kuhusu mateso yao mnamo mwaka 177 na huenda kama matokeo ya mateso yale, walihojiwa uasili wa Waphrygia au Wapega Wamontana [lakini wao wenyewe walikuwa hodari kwenye mitazamo au maoni yao na sio Mmontana (kwa mujibu wa kitabu kiitwacho Kitabu cha Maarifa cha Kikatoliki yaani, The Catholic Encyclopedia, C.E), art. Montanists, Toleo la X. kurasa za 522-523)]. (Montanus na manabii wakike Maximilla na Prisca au Priscilla walitabiri kwa maneno ya faraja huenda ni kwa ushawishi wa dhehebu la mafundisho mapotovu ya Cybele katika mji wa Phrygia au Pega. Wao pamoja na wafuasi wao walishutumiwa)
Irenaeus alikuwa ni M-unitariani, kama alivyokuwa Justin Mfia-dini na kama walivyokuwa Watetea-dini wote wa Ante-Nicene au Maguso wa Nikea. Alisema kuwa Kanisa lilikuwa na imani moja ya kudumu, kama vile kuna Mungu mwingine ila mmoja tu ambaye ndiye Muumba wa Ulimwengu, Mungu Baba (kwa mujibu wa jarida la ANF, Toleo la 1, la Kupinga mafundisho ya Uzushi yaani Against Hereses, Kitabu cha II, Sura ya IX, ukurasa wa 369). Alisema kwamba sehemu ya Kanisa ilikuwa ni:
Utakatifu mkamilifu ulihitajika kwa ajili ya maadhimisho halali yawayo yote. Hata hivyo sheria ya amri kumi za Mungu hazikufutwa na Kristo, lakini ni kwamba zinawamuru watu kutoziacha kamwe amri hizi za Mungu (ANF, Kitabu cha IV, Sura ya XVI. Ukurasa wa 480)
Ananukuu vitabu vya manabii Ezekieli (Eze. 20:12) na Musa (Kut. 21:13) akitaja kuwa hizi Sabato kuwa ni ishara kati ya Mungu na watu wake. Sabato zilitolewa ili kuwa kama ishara, ambayo pia ilikuwa ni alama. Sabato zinatufundisha kuwa tunatakiwa tudumu kila siku kwenye huduma tukimtumikia Mungu. Mwanadamu alikuwa hahesabiwi haki kwa ajili ya hizo, lakini zilitolewa kama ishara kwa waty wa Mungu (kama lisemavyo jarida lililotajwa hapo juu, ukurasa wa 481).
Ignatius, askofu wa Antiokia wakati wa utawala wa Trajan (miaka ya 98-177 BK), alipinga dhidi ya mitizamo ya Kiyahudi waliokuwa kwenye milki yake. Kudumu kwa mshikamano na heshima ya mambo yaliyoanzishwa ya Kiyahudi kama vile Sabato, yametajwa sana na mwandishi (kwenye Waraka kwa Wamagnesia, pia tazama kitabu cha Bacchiocchi, ukurasa wa 213). Kwa hiyo ni vigumu sana kufikirika kuwa ki chanzo cha kuivunja au kuzuia kutoka kuitunza-Sabato kuwa tayari kumeanza kuchukua mkondo wake (kitabu hicho hicho ukurasa wa 214). Hii kwa kweli ndiyo Ignatius aliyokuwa anazua matendo yenye kasumba ya mapokeo ya Kiyahudi siku ya Sabato ambayo ilikuwa ikitunwa na pande zote mbili.
Justin Mfia-dini, mwenyewe ambaye ni M-unitariani, ndiye aliyependekeza wazo la kufanyika kwa ibada siku za Jumapili (jarida la ANF, Toleo la 1, Ombi la Kwanza la Msamaha, LXVII, kurasa za 185-186) na akajaribu kumshawishi rafiki yake Myahudi Trypho juu ya usahihi wa tendo hili (kwa mfano, tazama kwenye ANF, Toleo la 1, Mahojiano na Ttrypho, Sura ya XII, ukurasa wa 200). Bacchiocchi (huenda ni kwa mamlaka juu ya kipindi cha mpito Kutoka kwenye maadhimisho ya Sabato hadi Jumapili, Chapisho la Chuo Kikuu cha Kipapa cha Wagregoriani cha Roma, 1977) huelezea kushinwa kwa Justin kutoa mifano iwayo yote ya huko nyuma ili kumsaidia kuhalalisha kutendeka kwa tendo hilo, madai ya Justin yalikuwa na sababu fulani nyuma yake katika kusema kuwa kwa wakati huu, maadhimisho ya Jumapili ni muafaka kwa Wakristo watokao sehemu zote mbili yaani kwa wanaotoka kwenye upagani na wanaotoka kwenye jamii ya Wayahudi (ukurasa wa 156). Pia Wanazarayo, hawakuadhimisha ibada za Jumapili, kama ilivyopingwa na Epiphranius (kwenye kitabu na kurasa huo huo). Wanazarayo, walikuwepo katika karne ya nne wanaelezewa na Jerome, wanaonekana kuwa moja kwa moja ni uzao wa jamii ya Kikristo ya Yerusalemu ambao waliingia huko Pella (Bacchiocchi, jarida hilo hilo na ukurasa huo huo).
Kusudi la kuwepo kwa hizi Sabato kulieleweka na waandishi wa kwanza kuwa ilikuwa ni ya kiroho ambavyo kwamba Wayahudi waliichukulia kwenye hali ya kimwili na hii ndio ilikuwa ni chanzo cha mijadala. Uondoaji wa Sabato na kuingizwa kwa Jumapili kungeweza kuzuilika.
Kanisa katika Lyons chini ya Irenaeus liliingilia bashishano kuhusu utaratibu wa maadhimisho ya siku ya 14 ya mlo wa Pasaka (tazama kitabi cha Butler kiitwacho Maisha ya Watakatifu, kurasa za 196-197; na pia majarida yetu yanayohusu Pasaka). Aliugawanya Ukristo wa kale kwa kiasi kikubwa na Gaul na kushughulikia kama kifo cha kupwa kwa hewa hadi kufikia muundo wa imani ya Wagnostiki ikijichimbia kule Lyons wakati wa Pontinus na Irenaeus ilikuwa ni kitovu cha Kanisa katika Gaul na ilikuwa ni kitovu uongofu.
Kiwango cha mateso yaliyofanyika huko Lynos na Vienne kilitolewa kwa ndugu wapendwa katika Smirna katika barua, ambayo ilitunzwa na Eusebius (soma jarida lisemalo Historia ya Kanisa au Hist. Eccl, V, I-iv). Mji wa Vienne ulikuwa unategemewa na mji wa Lyon na huenda ulikuwa unaongozwa shemasi (kwa mujibu wa nakala zinazoelezea kuhusu Wakristo wa Gaul, maarufu kama C.E., atr. Gaul, Christian, Vol. VI, p. 395).
Maknisa katika mji wa Gaul, yanaonekana kuwa yalikuwa yanasaidiwa na ushawishi mkuu wa Wayahudi waliokuwa karibu na miji ya marceilles na Genoa, kwa kipindi chote cha miaka ya 100-300 (tazama kitabu cha ramani cha Historia ya Wayahudi, maarufu kama Gilbert Atlas of Jewish History, Dorset Press, 1984, map 17). Watu wa jumuia hizi walikuwa kwa hakika katika mawasiliano ya karibu na kuhusishwa kikamilifu na Wayahudi waliokuwa katika miji ya Efeso na Smirna. Vuguvugu hili lililoelekea huko Rhone kutoka Merseille hadi Lyons kwenye miji mikubwa yaani Metrpolis na kiini cha mawasiliano kwa nchi nzima, bilashaka ni matokeo ya ushiriki wa Wayahudi katika shughuli za biashara. Mahitaji ya jamii huenda ndiyo yalilazimisha Pothinus na Irenaeus wapelekwe huko Lyons, kutoka kwa Polycarp wa Smirna. Kwa hiyo basi tunaona kuwa lilikuwepo Kanisa la Washika-Sabato lililoanzishwa huko Lyons mapema kabla ya mateso ya zama za Marcus Aurelius mnamo mwaka 177. Mji wa Lyons ulikuwa ni makao makuu ya makanisa yote yaliyokuweko huko Gaul kipindi ambacho Irenaeus alikuwa askofu. Makanisa ya Gaul yaliandika waraka na kuupeleka huko Roma kuhusiana na utata iliojitokeza kuhusiana na utaratibu wa kushiriki ushirika wa meza ya Bwana mara moja tu kwa mwaka (Quartodeciman), (tazama machapisho ya Hisoria ya Kanisa, maarufu kama Eusebius Hist. Eccle., V, xxiii) yanayowasaidia maaskofu wa Waasia kufanikisha kuanzilishwa na kuingizwa kwa Easter makanisani mwao.
Kwa mujibu wa Gregory wa Tours (jarida lake lijulikanalo kama Historia Francorum, I, xxviii) anadai kuwa mnamo takriban mwaka wa 250 Roma iliwapeleka maaskofu saba ili waende wakaanzishe Makanisa huko Gaul. Gatianus akaanzisha kanisa la Tours: Trophimus lile la Arcles: Paul akaanzisha lile la Narbonne: Stremonius (au Austremonius) akaanzisha lile la Auvergne (Clemont): na Martialis akaanzisha lile la Limoges (tazama maandishi yajulikanayo kama Lejav C. E. art. Gaul ibid). Kama asemavyo Lejav, swali hili liliulizwa sana na wanahistoria wote waliokuwa makini.ilikuwa ni zaidi sana ya ulingiliaji kati wa Warumi katika maamuzi ya mambo ya ndani ya mataifa mengine. Bila kujali nia ya dhati ya moyoni, Cyprian ananukuu kwamba katika zama za kipindi cha kati cha karne ya tatu, kulikuwepo idadi kubwa ya Makanisa yaliyokuwa yameanzishwa huko Gaul. Inaonekana kwamba mtawala wa wakati huo Costantius Chlorus, baba yake Costantine, hakuwa na uadui au chuki yoyote ile na imani ya Kikristo. Huenda ikawa ni kwa ajili ya hali hii ya mtangamano ya utegemezi wa Lyons, ndiyo ilimfanya Costantine akatae kuwa mfuasi wa mafundisho ya Athanasi (ambayo yalikuwa kwa sehemu yanaamini Utatu, na hatimaye wakaitwa Wakatoliki) na kwa kweli walibatizwa kwa imami tegemezi ya Unitarian (au kama ilivyokuwa ikijulikana kwa jina la Waeusebian.au Waarian) katika zama za mapema kabla ya kifo chake (tazama jarila la C.E., lililotajwa hapo juu na maelezo yake yote, na pia la uandishi uitwao vars wenye kichwa cha somo re Costantine). Baraza la kidini la Arcles linanukuu kuwa kulikuweko idadi kubwa ya parokia kuu (diocese) zilizokuwa zimeanzishwa kwa wakati ule (mnamo takriban mwaka 314) yakianzia sambamba na tangazo la Sheria mpya ya Mtangamano na mavimiliano (ya mjini Milan). Sahihi zilizowekwa na maaskofu hawa zingali bado zinadumu kuonekana, zikileta uhakikisho wa mabo yanayoonekana huko: Vienne, Marceilles, Arles, Orange, Vaison, Apt, Nice, Lyons, Autun, Cologne, Trier, Reims, Rouen, Bordeauux, Gabali, na Eauze. Madondoo ya Toulouse, Narbonne, Clermont, Bourges na Paris pia lazima yapelekwe (tazama maandiko ya C.E kama yalivyoelezewa hapo juu, ukurasa wa 396).
Imani ya kuishi mtindo wa kimonaki haikuingia kwenye Makanisa ya Gaul hadi pale ilipofundishwa na kuanzishwa na Martin (takriban mwaka 397), aliyeandisha au kujenga Jumba la kuishi watawa yaani Marmoutier karibu na mji wa Tours na Cassian (takriban mwaka 415). Akiwa pamoja idadi kubwa ya Wakristo wakiambatana naye kwenye miji, miongoni mwao wakiwemo watu wenye elimu na huenda wengine walikuwa ni Wayahudi walioleta ushawishi kwenye makundi mbali mbali. Wakazi wa maeneo ya mashambani walikuwa ni wapagani, wanaoamini Imani-potofu za Gallo na ushirikina wa Warumi. Uongofu wa Goths, Vandals, Suervi, Alans, nk, na kuingia kwenye imani juu ya Mungu mmoja wa pekee na wa kweli au U-unitariani (kimakosa sana imani hii iliitwa Arianism, yaani Uariani) tokea mwanzoni mwa karne ya nne, ikakomesha nia ya Warumi waamini Utatu na maadhimisho ya ibada za Jumapili kwa kipindi fulani. Madondoo ya kiaskofu ya Gaul, yakafanyika kuwa ni kiini cha mtungo wa kanuni ya imani ya kiaristocrat ikisimamiwa na ushawishi wa Kirumi. Honoratus akaanzisha makazi ya wamonaki katika kisiwa cha Lerins (Lerinum). Tokea hapo mamlaka ya kiaskofu yalichukuliwa na wale waliokuwa wanajulikana kama wanazuoni wahitimu wenye misimamo mikali wa Lerins ambao waliwekwa kwenye parokia kuu (diocese) zote. Kina Honoratus, Hilary na Caesarius waliwekwa kuongoza huko Arles; Eucherius akawekwa huko Lynos, na wanawe wakiume Salonius na Veranius wakawekwa Geneva na Venice ulioheshimika sana; Lupus akawekwa Troyes; Maximus na Faustus wakawekwa Riez.
Lerins kwa kiasi kikubwa ikawa ni chuo cha kufundisha elimu ya dini potofu za ulimwengu wa wapagani na elimu juu ya Mungu wa kweli yaani theolojia na ikaeneza mawazo yake ya imani ya kidini hadi kufikia maeneo yaliyoko mbali na kwa kina kwa kazi yenye maana kwa njia ya kimapokeo na kuhubiri kusikochanganyisha au kukubaliana na tamaduni potofu za watu na imani za kipagani zinazohusisha uwepo wa uwezekano wa kusaidiwa na wafu.
Kwa hiyo, shule za kimonaki zilianzisha mafundisho potofu ya kimizimu na kuyaingiza kidogo kigodo kwa kutumia hila za kidini kwenye kanisa la kwanza huko Gaul. Kukawa na upinzani wa dhahiri kati ya mfumo kiroho wa kiimani wa kimonaki na makasisi wengi walioa. Huu ulikuwa ni uzao au kizazi cha Merovingian, ambao hatimaye walianzisha utaratibu wa mfumo wa Kirumi hadi kufikia kiasi cha kulazimisha kwa upamga.
Hadi kufikia mwaka 417, wakati Papa Zosiamus alipomteua Ptrocles, askofu wa Arles, kuwa mwakilishi wake maalum wa huko Gaul, mabishano yalipelekwa huko Milan ambako Baraza la Milan lilitoa maamuzi ya mambo au kukata mashauri yote (tazama tena kitabu cha C.E., uk. 397). Kwa hiyo basi, ni rahiei kuona uhusiano kati ya Milan na maeneo mengine ya mbali ya Wasabbatati au Washika-Sabato au pia walijulikana kama Wavallenses. Makanisa ya Gaul yalikuwa kwenye mashindano au utata wa kimafindisho juu ya tabia na asili ya Mungu kwa kiwango kikubwa. Makanisa kwa wakati wote yaliendelea kuwa katika hali ya Utegemezi.
Kanisa la Gaul lilipitia kwenye vipindi vitatu vikuu vya mtafaruku wa mapokeo ya kimafundisho. Maaskofu wake walionekana kuwa na ushawishi mkubwa wa kuamini kwa kiasi kikubwa sana na mafundisho ya imani ya Arian; na kwa ajili ya kutimiza wajibu wa sheria tu zilizokuwepo, walionekana kama wapo kwenye imani ya mafundisho maazimio ya Nikea, licha ya mapungufu kadhaa nusu nusu na ya kipindi kifupi kifupi.
Hii huenda ilikuwa katika matamko. Wasabatati waliegemea kwenye mrengo wa U-unitarian moja kwa moja, tangia kuanzishwa kwake na kina Ponthinius na Irenaeus takriban kipindi cha zaidi ya karne moja kabla kusikika kwa Arius. Washika-Sabato walizidi kuenea katika nchi mbali mbali za Ulaya yote. Hefele anasema kuhusiana na Halmashauri ya Baraza la Liftinae lililokutana Ubelgiji mnamo mwaka 745 kwamba:
Sehemu ya tatu ya dondoo za kikao cha baraza hili inatoa onyo kuhusu maadhimisho ya Sabato, inkiiukuu marejeo ya makatazo yaliyopitishwa kwenye maazimio ya Laodikia (yajulikanayo kama Conciliengeshicte, 33, 512, kifungu cha 362).
Maadhimisho ya Sabato uliendelea kuwepo huko Roma hata zama za Gregory I (590-604). Gregory aliandika waraka akipiga marufuku maadhimisho haya [maarufu kama Ep. I, Nicene and Post-Nicene Fathers (NPNF), Second Series, Vol. XIII, p. 13, yaani matendo ya Makasisi wa zama za Mtaguso wa Nikea na baada ya Mtaguso wa Nikea], unsema hivi:
Askofu Gregory, aliyepewa wadhifa huu kwa neema ya Mungu, kwa ndugu zake wapendwa, wakazi mnaoishi Roma. Imetokea kwangu kugundua kwamba kumekuweko na watu fulani wenye roho zilizopotoka wamejiipenyeza miongoni mwenu na kuwafundisha na kueneza mafundisho na mambo mapotofu na kuwapoteza kupingana na Imani Takatifu, na kwamba wanafundisha na kuwakataza watu wasifanye kazi au kitu chochote kufanywa siku ya Sabto. Je, mimi nitawaita jina gani watu hawa kama sio Wapinga-Kristo (kwa mujibu wa waraka ujulikanao kama Epistles, b. 13:1).
Gregory alitangaza fatwa ya masusio dhidi ya mji wa Roma na wakazi wake, kwa sababu walishika Sabato. Alishikilia kuamini kuwa wakati mpinga-Kristo atakapokuja, basi atafanya maadhimisho ya ibada ya siku ya Jumamosi kama Sabato (ukisoma waraka huo huo).
Kanisa la Kisabato katika Asia
Kanisa lilianzishwa katika Asia Ndogo ambako lilijulikana kama la Wapaulician. Wapaulician walijiendeleza kule kwa kipindi cha miaka mamia kadhaa. C.A Scott aliwaelezea hivi hawa Wapaulicians kwamba walikuwa hivi:
Ni imani ya watu wanaopingana na Ukatoliki ambayo ilianzishwa kuanzia takriban kwenye karne ya 7 (na pengine mapema kidogo huko nyuma) waliopitia kwenye uzoefu wa nyakati mbali mbali za mabadiliko mengi yakiwemo upendeleo wa nguvu za dola na vipindi vya mateso makali sana na yasiyo na huruma wakibakia kuwa na ushawishi mkubwa hadi kufikia karne ya 12; na hawakosi kuwa wanao uzao na umoja na watu walioko Ulaya Mashariki hadi kufikia leo. Inaonekana ilitokea kwa mara ya kwanza upande wa mashariki ya ukingo wa mpaka wa dola, na kuwa imani hii inamakazi yake ya asilia katika Mesopotamia na Kaskazini mwa Syria, kasha ikaenea kidogo kidogo kwa njia ya propaganda kwa kidogo kidogo imejipandikiza na kuota mizizi, ikielekea pande za magharibi ikipitia Asia Ndogo, hatimaye pande za Mashariki mwa Ulaya ili kuanzisha karne mpya katika eneo la mkono wa bahari wa peninsula ya Balkani. matukio maalumu zinazoonekana kuhusishwa nayo ni yanajumuisha na mawazo mchanganyiko ya aina mbili ya kiutawala kama sio yahusuyo mwanzo au chanzo cha kuwepo kwa ulimwengu, mafundisho ya Wanaoamini juu ya mabadiliko ya kimaumbile Ubinadamu wa Yesu, wakorofi na wagumu wa mioyo wakataao kumtukuza Mariamu na kuomba watakatifu na kuabudu sanamu, pia kwa jinsi hiyo hiyo hukataa imani juu ya mfano wa sakramenti, na wanasisitiza kwa namna ya kipekee juu ya ubatizo wa watu wazima kuwa huu ndio pekee ulio halali katika utaratibu wa kimaandiko. Misingi ya uwezekano huu unapatikana katika tafakari za Maandiko Matakatifu kama ndio pekee na yanayojitosheleza katika kupinga na kuondoa taratibu zote za kimapokeo na kile kinachoitwa ‘mafundisho ya kanisa’ (tunasoma haya katika kitabu kiitwacho ERE, art. Paulicians, Vol. 9, p. 695)
Wapaulician waliongezeka kwa kasi kubwa sana idadi yao chini ya uongozi wa Sergius Tychicus na walipatikana kwa kiasi kikubwa kwenye watu wagumu wa milimani ya Taurus.
Scott anaendelea pia kusema kuwa: ni kama vile walivyo walinzi wa dola na kama kiini cha mateso yatokanayo na nguvu ya dola, walionekana kuwa na unyenyekevumu mkubwa na ujasiri (soma haya kwenye kitabu hicho hicho, uk. 697).
Walilindwa na Costantine Copronymous (741-775) na kualikwa kwenda kuweka makazi huko Trace. Nicephorus (802-811) aliwaajiri kwa ulinzi wa dola kwa upande wake wa mashariki. Michael na Leo V waliwatesa bila ya huruma kabisa.
Lakini Wapaulician walikuwa ni wengi sana, na wapenda vita sana na ni wenye uwezo mkubwa sana wa kupangilia mambo waliojipanga vizuri ili kumezwa kwenye imani kali. Walizuia, wakaasi na hata walijilipiza kisasi cha maovu kwa kuishambulia Asia Ndogo kwa kutumia milima iliyo mirefu na kwa kasi. Baada ya miaka ishirini ya mlinganisho wa utulivu walionekana kupitia kwenye mateso makubwa zaidi chini ya Theodora (mnamo mwaka 842-857), ambayo chini ya Basil iliendelea hadi kufikia kiwango cha vita isiyokoma (tazama Krumbacher, p. 1075). Wapaulician walifukuzwa kwa mikono ya Saracens, huku akiwepa msaada na wao, chini ya uongozi wa mtawala aliyekuwa mwenye uwezo Chrysocheir, si kwamba hawakuweza tu kuyazuia majeshi ya dola hii ya kifalme, bali waliyasukumilia mbali nyuma na kuifanya Asia Ndogo hadi kufikia ukingo wake wa fukwe za Magharibi (kitabu hicho hicho cha Scott).
Hii inaonyesha mambo mawili kuhusu Wapaulician. La kwanza ni kwamba walitumia mikono na la pili ni kwamba Waislamu waliwachukulia kama ni kikundi kilicho tofauti na Wakristo wengine wanaoamini juu ya Utatu na kinachohitaji msaada wao wa kiulinzi. Ulinzi huu haukuhusishwa katika Asia ndogo, bali uliendelea hadi Uhispania. Tofauti kati ya makundi haya ilijulikana na kulindwa atika Koran.
Ushauri wa Kristo kwa Kanisa la Pergamo, ambao unapaswa ujulikane na kikundi hiki cha kiimani, ni kule kunakofanya iwe yenye kuingia maanani ni pale asemapo hivyo katika Ufunuo 2:16, kuwa atapigana vita na wale wote [wayashikayo ya uongo miongoni mwao] kwa kutumia upanga wa kinywa chake.
Scott anachukulia ule uhamisho wapili wa Wapaulician, katika mtazamo mpana sana kuanzia Armenia hadi Thrace, uliofanywa na John Tzimiskes (mnamo mwaka 970) (kama isemavyo hapo juu). Wapiganaji waliojulikana kama (Latin Cruseders) walianzisha kikundi cha kidini huko Syria katika karne ya kumi na moja na Mwanamke aliyejulikana kama Mariamu Montagu, aliwakuta kwenye ukingo jirani wa Philippoplis, mnamo kwenye karne ya kumi na nane (Scott, op. Cit).
Baani Ulaya waliendelea hadi kufikia au waliunganishwa na Wabogomi (q.v), na mtazamo wao mvuto wao ulitangazwa kuenezwa kwa kipindi chote cha Zama za Kati na vikundi mbali mbali vilivyosimama kinyume na imani ya Kikatoliki- kwa mfano, Wakathari, Waabilgene – ambao walikuwa na muunganiko tangamano na Wapaulician ni pengine ni vigumu sana kuwadhania. Majina yao kama ‘Manichaean’, walibadilika kwa maelekezo ya kiuzaliwa wa vikundi vyovyote kati ya hizi vilivyopinga maendelezo ya madaraka ya kiwadhifa ya Ukatoliki na mafundisho yake (tazama kitabu hicho hicho cha Scott).
Scott anasema kuwa ni vigumu sana kujua ni nani hasa kati ya Papa Licani, wa kabila la Piphles wa Flanders, au Publicani, aliyeshutumiwa na kutangazwa vibaya huko Oxford mwaka 1160, ambaye moja kwa moja alitokana na Wapaulician, au kuchukua jina lao kama kama alama ya mashutumu. Scott anasema kuwa Wapauliciani, ni waelewa wazuri mno kama watendaji, kwa jinsi hiyo ya mlolongo endelevu wa kupinga imani ya Kikatoliki na upingaji wa mawazo ya mgawanyo wa kimadaraka na kimaisha, ambao unaendana kwa wakati mmoja na mwenendo wa mafundisho ya ‘kihafidhina’ na mfumo wake, kimatendo kwa wakati wake wote wa historia ya Kanisa (tazama Crumbacher, p. 970,the Paulicians’ setzten einer verweltlichen Reichsorthodoxie ein echt apostolisches Biblechristentum entgegen).
F.C. Conybeare (katika jarida lake la The Key of Truth, yaani Mlango wakuelekea kwenye Ukweli. kilichochapishwa huko Oxford, 1898) anasema kwamba watu hawa walikuwa ni watu Waliojiingiza kwenye mafundisho ya Ukristo; wakiamini kuhusu sacrament tatu kuu yaa ni za toba, ubatizo na za Mwili na Damu ya Kristo (pia angalia ukurasa wa 124), wakatangaza kuwa ubatizo wa watoto wadogo haupo na kupiga marufuku, wakatangaza kusimama kinyume na imani juu ya uwepo wa daima wa ubikira wa Mariamu, na kuyakataa mafundisho ya uwepo wa wafu huko toharani na maombi ya kuwaomba watakatifu, na matumizi ya taswira za aina mbali mbali yaani michoro ya picha, misalaba na matumizi ya ubani.
Kwa hiyo basi, maendeleo ya Kanisa kutoka Asia Ndogo kuingia Ulaya, yaliendelea kwa kipindi cha karne mbali mbali kadhaa na kama inavyoonekana hapo juu, waliathirika na maneno ya kutoka midomoni mwao na utaratibu wa kimakazi wa watu wao. Upandaji wa mafundisho ya kimakundi ulifanywa na wahafidhina ambao kwa kiasi fulani, wameandika historia ya jambo lenyewe.
Washika-Sabato wa Ulaya ya Mashariki
Ni jambo lililo dhahiri kabisa kuwa, kazi kubwa sana ya Makanisa Yanayoishika-Sabato, haikuanza huko Ulaya hadi kazi za makanisa ilipoanzishwa kutokea Smirna (kama inavyojulikana kuwa ni zama za Wasmirna) na kwa wale walioingia wakitokea Upaulician katika Asia Ndogo (wakijulikana kama zama ya Wapergamo) waliendeleza shughuli zao. Kwa kweli ilikuwa kwamba kazi katika Gaul ilikuwa imeanza kutikea na mawaailiano Makanisa ya Smirna, hadi pale kufikia baada ya kifo cha Irenaeus. Kazi ilikuwa haijawa katika muunganiko mzuri na utaratibu sawia, hadi kufikia uwekaji makazi wa Wapaulician katika Ulaya.
Ueneaji wa imani ya Wakristo Wanaoshika-Sabato (kama inavyoonekana hapo chini) ulionekana kuendelea kutoka Thrace kuelekea Albania na Bularia, na Wapaulician. Mnamo kwenye karne ya tisa mabishano haya yakafika Bulgaria. Inaaminika na kunukuliwa kama hivi kwamba:
Katika enzi ya kipindi chake cha siku za mwanzo wa Uinjilishaji, Bulgaria kulifundishwa kwamba hakuna kazi iliyokuwa inaruhusiwa kuanyika katika siku ya Sabato (haya tunasoma kwenye majarida yaitwayo Responsa Nicolai Papae I na Con-Consulta Bulgarorum, Responsum 10, yaliyokutwa huko Mansi, Sacrorum Cocrorum Concilorum Nova et Amplissima Cellectio, Vol. 15, p. 406, pia Hefele, Conciliengeshict, Vol. 4, sec. 478).
Bongari, mtawala wa kifalme wa Bulgaria, alimwandikia Papa Nicholas I orodha ya maswali kuhusiana na jambo hili. Jibu kwa swali la 6 kuhusiana na kuoga miili na kufanya kazi siku ya Sabato, lilikuwa ni kama ifuatavyo hapa chini:
Swali la 6 kuhusiana na suala la Kuoga miili kunaruhusiwa kufanyika siku ya Jumapili, lakini sio pia kwa siku za Sabato (Hefele, 4 346-352, sec. 478).
Nicholas aliyangazwa kuwa ametengwa na kanisa na sinodi ndogo ya Costantinople. Photius, aliyejulikana kama baba za kanisa la Costantinople alichongea kenye ofisi ya Papa akisema kuwa:
Jambo hilo ni kinyume na kanuni, waliwafanya Wabulgaria wafunge saumu siku ya Sabato (Photius, von Kard Hergenrother, 1.643).
Swali kuhusu ninini iwe siku ya Sabato lilikuwa ni mabishano makali kati ya Wayunani na Wataliano. Neale alitoa maoni yake yakuunga mkono jambo hili kukipelekea kugawanyika kati yao mnamo mwaka 1064 (kwa mujibu wa jarida lisemalo Historia ya Kanisa Takatifu la pande za Mashariki, au A History of the Holy Eastern Church, Vol I, p. 731).
Waathingian (au Athingani) wa karne ya tisa walishawishiwa na Cldinali Hergenrother, wasimame kwenye mahusiano ya karibu sana na Mfalme Michael II (miaka ya 821-829) na inasemekana kwamba walikuwa wakiishika Sabato (kwa mujibu wa jarida la Kirchengeschicte, 1, 527). Waathingani walikuwa ni kikundi cha kidini waliokuwa huko Phrygia, walioaminika kuwa walikuwa ni uzao wa Melkizedeki kwa mujibu wa jarida lililoandikwa na Timotheus wa Costantinople linaloelezea kuhusu Kupokelewa kwa Mafundisho ya Upotovu (tazama jarida la ERE, art. Sects, Vol. XI, p. 319b). Utaona jinsi Whitley anavyoelezea hapo kuwa:
Wale walioitunza siku ya Sabato, kwa kadiri ilivyokuwa kwamba hawakumhusisha mtu yeyote, walijulikana kwa jina maarufu kama Waathingani. Hii huonekana kana kwamba walizishika sheria za Kiyahudi zinazohusu mambo ya usafi, lakini maelekezo yake yameadimika sana kuweza kusaidia kupata kueleweka chanzo chao na misingi yao ya imani (Soma jarida hilo hilo lililoelekezwa hapo juu).
Baada ya kushindwa kwa Chrysocheir, kiongozi wa Wapaulician mnamo kwenye karne ya tisa, na kuangamia kwa mji wa Tephrike, uliokuwa ngome yao, walifanya mauaji makubwa na wakatawanyika. Walidumu kuwepo kwenye jumuia zilizotawanyika za huko Armenia, katika Asia ndogo na hasa hasa kwenye Ufukwe wa Peninsula ya nchi za Balkani. Katika siku za kati kati ya karne ya tisa, walijionea uamsho huko Armenia ukiletwa na Smbat, ambaye kwa mujibu wa Conybeare yaonekana huenda alikuwa ndiye aliyeandika kitabu au jarida lijulikanalo kama Chanzo cha kukuelekeza kwenye Ukweli kwa Kiingereza husomeka kama Key to Truth (soma jarida hili la ERE, art. Paulicians, Vol. IX, p. 697). Makao yake makuu yaliwekwa katika mji wa Thondrak, wakapewa jina wakaitwa Wathondrakia.
Tawi lingine kutokea kwenye chanzo hicho hicho huenda ni lile linalopatikana kwenye kikundi cha imani ya kidini kinachojulikana kama ‘Anthingani’ kikihusisha na Theophanes (kwa mujibu wa jarida la Chronographiaofia, 413), na pia jingine katika ‘Selikians.’ Mchunguzi wa mambo ya mababa wa imani aitwaye Methodias anadai kustahili kwake kushukiwa kuwa miongoni mwa watu wenye msimamo mkali wa kihafidhina mmoja ni Felix na wafuasi wake, ambao walishikilia kuamini kuwa mawazo-tegemezi ya ‘Manichaean’ ambayo kwa inahusiana na mashutumu yaliyowakabili Wapaulicians katika jarida liitwalo Cod. Scor. (kwenye jarida hilo hilo).
Uhamisho wa pili wa kupelekwa utumwani chini ya John Tzimiskes (970) alivyoonekana baadae.
Kwa hiyo basi inaonekana kuwa vikundi hivi vya kidini vilikuwa na mahusiano fulani ya kimafungamano na yalishutumiwa kwa kuonekana kuwa yalikuwa na mafundisho potofu na kuonekana hivyo na waamini Utatu hivyo basi yakamomonyoka na kuwa vikundi mbali mbali kimajina na kuteswa kwa kadiri ilivyowezekana. Wapaulician pia walikuwa wavumilivu katika hali hii na waliendelea kudumu kwenye imani ijulikanayo leo kama Sabbatati na Cathari katika Ulaya.
Mara zote Wapauliciani walikuendeleza kushikilia imani yao ya kuabudu Msalaba (kwa mujibu wa ushuhuda wa Waarmenia na Chazus), kwa hiyo, neon Chazitzarii, Chazinzarians (Staurolatrae) yanaashiria kuonekana kuwa hakikuwa kikundi kigodo cha watu walioshikilia imani hii, bali lilikuwa ni Kanisa lililoanzishwa kwa mwelekeo mzuri huko Armenia kama lilivyoonekana na Wapaulician (kwa mujibu wa jarida la ERE, art. Sects, p. 319).
Troitsky kwenye jarida lake aliloandika kuelezea Kanisa la Wahafidhina la Kiyunani (jarida liitwalo ARE, Vol. VI, p. 427), anaonekana kuwaelezea Waathiangani kuwa walifanishwa na Wayahudi. Walifungamanishwa nao, lakini hawakuelezewa kwa uwazi kama ni Wapauliciani. Troitsky anaonekana kuwaunganisha Wapaulician kuwa ni kama watu waliokuwa na imani yenye tabia zenye mchanganiko wa mambo yakisirisiri, tunayoyashuku kuwa hayapo sahihi, kuanzia kwenye kazi zilizoanzia. Wakionekana kuwa na mashaka kidogo kuwa Wapauliciani na Wapauliciani na Waathingani, au vikundi vya kidini vilivyokuweko Asia Ndogo, waliitunza Sabato na sheria ya vyakula vipasavyo kula na waliyapeleka mafundisho haya hadi Ulaya.
Wabogomili
Mojawapo kati ya makundi yaliyotokea kwa Wapaulician moja kwa moja katika Ulaya, inaonekana kuwa walikuwa ni Wabogomili (kama inavyoonekana ukitazama hapo juu) waliotokana miongoni mwa Waslavs na hasa hasa Wabulgars (kwa mujibu wa Powicke ERE, Vol I, p. 784).
Jina la Wabogomili huenda lilitokana. Muungano wa maneno mawili yaani Bog Milui yenye maana kuwa Mungu na aturehemu, au huenda ni Bogomil au ndugu waliopendwa na Mungu. Wabulgaria wawili wa siku za mwanzo MSS, waliothibitishana, walisema kuwa ‘papa’ Mbogomil alikuwa ndiye wa kwanza kufundisha ‘mafundisho ya upotovu’ maarufu kama heresy akiwa chini ya M’bulgaria Tsar Peter (kwenye miaka ya 927-968). Kwa hivyo basi inawezekana kuwa jina hili limetokana ama kuchukuliwa kutoka kwa mmoja wapo wa viongozi maarufu wa siku za nyuma yao aliyekuwa kiongozi wa imani hizi za kidini, kwenye karne ya kumi.
Wabogomil walifahamika kama Wamanichaean waliokuwa kwenye imani yenye mtazamo wa kimamboleo, kwa mujibu wa maelezo ya N. A. Weber (jarida lake maarufu kama C. E. art. Bogomils, Vol. II. P. 612). Kikundi hiki cha kiimani kinaaminika kama kilianzishwa kwenye miaka iliyofuata baadae kwenye Zama za Kati huko Costantinople na kwenye maeneo ya majimbo ya Balkani. Wabogomil walishikilia kuamini kwamba wote wawili yaani Shetani na Kristo walikuwa na uweza sawa katika uumbaji, kwa mamlaka na mapenzi ya Mungu. Wabogomil waliamini kuwa Mungu Baba alikuwa na mwonekano wa umbo la kibinadamu lakini alikuwa hawezi kukamatika. Wana wa Mungu akiwemo Sataneli (au Azazeli), waketio kwenye mkono wa kuume wa Mungu, na Yesu au Michael. Shetani alikirimiwa uweza wa kuumba, lakini aliasi. Akiwa pamoja na malaika wote waliomfuata, alitupwa chini kutoka mbinguni. Iliaminika kwamba Shetani aliziumba mbingu ya pili na nchi ya pili na kumfanya mwanadamu kutoka katika mavumbi ya nchi na maji. Shetani akashindwa kumpa mwanadamu roho yenye kumpa uweza wa kuwa nafsi hai. Hivyo basi, Baba akampa huyo mwanadamu uweza wa kuwa ni nafsi hai baada ya wao kumuomba afanye hivyo. Kupitia na maelelezo ya Hawa, Shetani alipoteza majaliwa yake ya uweza wa uumbaji, lakini bado alifanya na kuendeleza mahusiano yake na wana wa sayari hii. Mungu akamtuma Mwana wake mwingine, Yesu, auchukue mwili wa kibinadamu kupitia njia ya kuzaliwa kwa tumbo la Mariamu. Kwa hiyo, Shetani akahukumiwa kwa njia matendo ya Kristo. Satanieli akapoteza jina la kimbinguni au uungu halali maarufu kama El hatimaye akageuka kuitwa jina baya la Shatani kama anavyojulikana.
Sasa basi, habari hii imeandikwa na “maadui” na kwa kiasi fulani kuhusianisha na mfumo wa kihistoria unaohitaji kufafanuliwa. Hatahivyo, wasomaji wa Biblia wataona utaratibu vifungu vya maandiko matakatifu ambayo yameenezwa. Fikra hii kwakweli ni zaidi sana katika uwiano, kwa vile tuonavyo sasa kwa elimu ya mambo ya ulimwengu ya zama za karne ya kwanza, lakini ikigubikwa na kama inavyoelezewa na Powicke (hapo chini) ni sawa sawa.
Dhana yengewe ni ile iliyoendana sambamba, kwa mtu wa pekee aishiye mbinguni, ambaye ni Mungu Baba, ambao kwa wote wawili yaani Kristo na Shetani wanahusishwa. Hii ndiyo maana ya kusema kuwa Mungu ni yote katika yote. Dhana hii pengine imefafanuliwa kwa namna iliyo rahisi sana na wahafidhina, kwa sababu haihusiani na fundisho la roho.
Madai ya Weber, ambayo Wabogomili waliolikataa Agano la Kale zaidi sana kuliko ilivyokuwa Wapsalter na vitabu vya kinabii, inaonekana kuegemea kwenye Euthymius (kwa mujibu wa PG, Vol. Cxxx) (tazama pia Powicke, op. cit) ambako kuna vichwa 52 vya kanuni za imani, nyingi kati ya hizo ziliorodheshwa na Powicke na kuainishwa kwa mintaarafu kama ifuatavyo:
1.Kukataliwa kwa vitabu viliyoandikwa na Musa.
2. Historia ya Kristo ni ishara ya ujuzi wa kiwango cha juu sana kuliko uwaowote.
3. Walifundisha mafundisho ya Wabellian kuhusu Uungu wakisema kwamba majina yote matatu ya Baba, Mwana na Roho Mtakatifu yanamhusu Baba yeye yule. Hatimaye huko mwishoni roho zote tatu zitafanya kazi zake zitakabidhiwa kwa Baba. (Wazo la kusema kwamba watawakilisha kwa Baba halikuwa na uhusiano na fundisho la Utatu kama ilivyo dhana ya Euthymius alivyodai kutokana na mafundisho yanayohusisha imani kuhusu ushirika kati ya watakatifu waliohai).
4. Uumbaji wa Kishetani uliendelea kwenye sheria ambazo zilizaa matendo ya dhambi. Mungu akaingilia kati hapa duniani na kumtuma Malaika Mkuu Michael kama neno ambalo lilifanyika kuwa ni Yesu Kristo.
5. Roho Mtakatifu aliaminika kukaa ndani ya wateule tu (ambao ilifananishwa na Wabogmili).
6. Walifundisha pia kuwa wateule hawawezi kufa.
7. Walishikilia kuamini na kufunsha kuwa mahekalu au majengo ya Kanisa yalikuwa ni mahekalu ya mapepo na mashetani lakini waliruhusu kufanyika kwa ibada sehemu ile kinyume na matarajio yao.
8. Waliaminika kufikirika kuamini kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ni mtumishi wa Mungu wa Wayahudi aliyeitwa Sataneli.
Ilidaiwa pia kuwa kundi hili la kiimani liliukataa ubatizo wa maji na kushikilia ubatizo wa kiroho pekeyake (uliofanywa kwa njia ya kuwekea watu mikono juu yao), ambao huenda ikawa ulichukuliwa kutokana na kuingizwa kwa nguvu kwa imani zilizoaminika katika mifumo ya vikundi vya watawa wamonaki. Kundi hili pia lilikataa mafundisho kuhusu hali yakujinyima au kuepukana na ulaji wa vitu vilivyoharamishwa. Weber alielezea kwamba kikundi hiki pia kiliharamisha mambo ya kuoa na kuolewa na walikataza ulaji wa nyama. Imani hii ya Wabogomili iliendelea kwa vipindi vya karne nyingine nyingi kadhaa, ikifuata mfumo wa kimonaki. Na kwa kadiri vile maandiko yao yalivyokuwa yakichomwa moto, kwa kile kilichokuwa sasa kinajulikana na kuonekana nao wenyewe kuwa ni kilichukuliwa kutoka kwa Euthymius Zigabenus (aliyefariki baada ya mwaka 1118) kwenye Sura ya xxvii ya jarida lijulikanalo kama Panoplia Dogmatike ambamo alikanusha mambo ishirini na manne miongoni mwa baadhi ya madai yao waliyoyaita kuwa ni mafundisho ya uzushi (chini ya vichwa 52 kama vile Powicke).
Weber alichukulia kuwa Wabogomili huenda walianzia kutoka kwenye imani ya Waeuchite (huenda ilitokana na tabia yao ya mabadiliko kuwili ya mafundisho yao). Pia waliitwa Wamessaliani ambako walichukua imani yao inayoshikilia misimamo mikali ya kujinyima na kujiepusha na mambo ya ulimwengu yaani uascetisism. Mabadiliko haya ya tarehe hii isiyojulikana, yanaonekana kuwatenga wao mbali na makundi mengine. Umaarufu wao ulizidi kujulikana mnamo katika karne ya kumi na mbili. Kwa mara ya kwanza walitajwa kwa jina huko Philippopolis (ikimaanisha Waturuki Wazungu) mwaka 1115 (walijulikana kuwa waliendelea kuweka makazi yao na Wapaulician hapa kama ilivyo hapo juu). Kiongozi wao Basil, aliyekuwa mtawa wakiume na tabibu, ambaye alichagua mitume kumi na wawili, alitiwa mbaroni kasha kufungwa jela (mwaka 1111) baada ya kufanyiwa hila) na Alexius I, Comnenus (mwaka 1081-1118) ambaye alidai upigaji marufuku wa makosa. Baadhi yao walikatazwa, baadhi yao walifia magerezani (kwa mujibu wa jarida la Weber hilo hilo). Basil alihukumiwa kifo mwaka (1118) na maiti yake kuchomwa moto mwaka (1119 asema Powicke). Synod au Parokia ya Costantinople katika mwaka 1143, maaskofu wawili wa Cappadocia waliondolewa madarakani kwa ajili ya kutatiza mafundisho ya imani. Synod za Costaninople katika mwaka wa 1316 na 1325 pia walishutumu makundi haya ya kiimani. Wabongomili walibakia hadi kutwaliwa kwa nchi za Balkan na Waturuki kwenye karne za kumi na nne na kumi na kumi na tano (kama asemavyo Weber hapo juu). Powicke anasema kwenye jarida lake maarufu la (op. cit., p.785) ushawishi wake unapenyeka, kwenye jumuia ndogo zaidi ambayo kwayo walitawanyikia, kwa nyakati za baadae sana. Kinachoonekana kuwa ni jambo ni kile ambacho mafundisho ya Wapauliciani kwamba sio kwamba yalikuwepo kwenye jamii ambako walipelekwa na katika jumuia ya Slavic, waliowazunguka lakini walichukuliwa na utaratibu wa wamonaki, ambao walibadilishwa na watawa wakiume, lakini hata hivyo, wapinga imani na mafundisho ya Ukatoliki. Mafundisho ya Wabogomili kama walivyopelekewa, wakiwakilisha michepuko kutoka kwenye imani nyingine za kidini, ikichukuliwa kutoka kwenye Upauliciani na kwa kweli kutoka kwenye mafundisho ya Wapauliciani wenyewe.
Kwa hiyo sasa ni makosa, kuwa imani hii ya kidini miongoni mwa utaratibu wa kimonaki, kama Wabogomili, ambako kwa kweli vikundi vya jumla vya majina yale, ambao yalisambaa na kuenea kati ya Waslavs na katika Ulaya yote. Mtazamo mkuu wa mafundisho yake unaweza kuwa mwanzo mzuri wa msingi na mfano wa kulinganishwa kati Wapauliciani na imani za kidini za watu wa Ulaya, ambao ulipata ushawishi na wao.
Waelekevu tegemezi ambao, au wapinga imani ya madhehebu yanayoamini Utatu, walioenea kuelekea Ulaya yote nzima. Imani hizi za kidini yalijulikana kwa majina mbali mbali tofauti.
Waaldensia au Waaldenses
Lentolo ni mwandishi wa zama za historia ya Waaldensia na mwenye mamlaka kwa ajili ya mateso ya wakati wake ule. Historia hii haikuwa dhahiri hadi kufikia mwaka 1897 Comba aliweka ushawishi mkubwa kwenye nakala yake kwenye Maktaba ya Berne (kwa mujibu wa W.F. Adeney, art. Waldenses, ERE, Vol. 12,p. 669).
Kwa hiyo, historia iliyoandikwa na Muston jarida liitwalo (L’Israel des Alpes, Paris, 1851, au Eng. Tr.and reprint Israel of the Alps NY 1978) ni lazima itazamwe kinyume chake. Kanisa Katoliki la Kirumi linadai kwamba Waaldensian walikuwa ni wafuasi wa Peter Waldo wa Lyons. Jina lililopewa kwa Kifaransa ni Valdes, kwa Kilatini ni Valdesius, Valdenius, Gualdensis na Kitaliano kama Waldo. Alidaiwa kuingia kwenye wongofu mwaka 1173. Waaldensia wenywe walikataa madai haya, ambayo kwa umuhimu waliwaweka alama ya Kiprotestant, na kuwaweka wazao wake nyuma ya Ukristo halisi uliokuweko huko nyuma.
Nukuu za madai ya kale sana yahusuyo madai ni ya mtawa wa kiume Mdominicana wa Passau mwaka 1316 (jarida la Contra Valdense katika sehemu isemayo Maxima Bibliotheca veterum Patrum, Lyons, 1677-1707, xxv, 262 ff), inanukuu kwamba wanaaminika kuwa walikuwepo kwa wakati wa mababa jarida liitwalo (duravit a tempore patrum). Wakati mwine ujao inanukuliwa, ni kutokana na waraka wa Barbe Morel akimwandikia Oecolampadius mnamo mwaka 1530 (kwa mujibu wa A. Scultetus Annalium Evangeli…decades duo, Geneva, 1618, pp.295,306). Maandiko haya yaliigwa na Robert Olivetan na kuchapishwa kwenye kurasa za mbele kwenye tafsiri zake za Biblia mnamo mwaka 1535. Kwa hiyo basi, Waprotestant walikuja kuwaheshimu Waaldeansi, kama Kanisa moja inalindwa na imani ya kanisa la Agano Jipya. Kikundi hiki kiliwaita viongozi wao Barbe au Uncle yaani Babe au Mjomba, kwa ajili ya agizo la Biblia linalokataza watu kumuita mwanadamu hapa duniani kumwita baba, mwalimu au kiongozi (Mat. 23:9-10). Jina au cheo cha kumuita mtu Baba kilikuwa ni cheo cha kiongozi katika utaratibu wa kikundi cha imani ya Mithra na ulikatazwa kabisa kutumiwa kwenye Ukristo (tazama mfano wake katika C.K. Barrett jarida lisemalo Asili ya Agano la Kale: Makabrasha yaliyochaguliwa; yaani The New Testament Background: Selected Documents, rev, ed, SPCK, London, 1987, p133). Bado hakujawa na ushahidi kuthibitisha kama kikundi hiki bado kilikuwa kinaendelea kuwepo, kisibadilike, huko kwenye mabonde la Alpine. Kwa kukubalika kwao kwa ajili ya ukweli huu, basi ufafanuzi wa dhana ya pili katika kufafanua kuhusu kikundi hiki cha kiimani kuliendelea. Dhana hii inaaminika kuwa ilianzia Roma, wakati ambapo hatamu ya madaraka ya kiaskofu ilishikiliwa na Sylvester. Inaaminika kuwa Sylvester, ambaye baada ya ubatizo wa Costantino [ambaye alidhaniwa kimakosa kuwa kama alivyokuwa Costantine kuwa alibatizwa kwenye imani ya Waunitariani (ambao kimakosa waliitwa Waeusabiani au Waariani) na Eusabius wa Nicomedia] aliyelitia Kanisa kwenye mamlaka ya mtawala. Ilidaiwa kuwa askofu alivunjilia mbali na kwenda na kwenda kwenye Bonde la Vaudos, kisha wakaanzisha kundi la Waaldensia. Kwa hiyo, hata hivyo, uwezekano wa Waariani Wagoths, waliokuwa na Biblia waliokaa Goths kutoka mwaka takribani kama 351, waliwavutia maeneo yale. Mwanzo wa Kanisa kwakweli, ilipingamizwa na Kanisa la Lyons, chini ya Irenaeus na warithi wake (kama isemavyo hapo juu). Mwanzo wa ushawishi bado unaonekana katika zama za Claude, askofu wa Turin katika karne ya nane, chini ya Charlemagne na Louis Mnyenyekevu. Claude alifufua mafundisho ya Waaugustinian ya kukusudiwa tangu mwanzo, lakini ilidharau mamlaka ya Juu ya Kanisa ya Mafundisho ya Augustine,
Kwa mujibu wa namna ile Kanisa lilivyokuwa ni kiunganisho cha kati kimawasiliano kati ya Mungu na mwanadamu, likipingamiza madai ya kipapa na kukataa mafundisho yasemayo kwamba mtakatifu Petro kuwa alipewa uweza wa kufunga jambo na kufungulila. Alikuwa na misalaba pamoja na sanamu za kuchonga zilizoondolewa kutoka makanisani, na mambo haya yote yanatarajiwa Mageuzi (tazama jarida la Adency, kama lilivyo hapo juu).
Makanisa ya Wavaudos, waliaminika kuwa alijumlishwa na parokia au diocese za Claude. Kwa mujibu wa Leger, Muston na Waaldense, walishikilia kwamba kama haliyao ya kuchukulia mambo kutoka pahala pengine kusingeweza kufanyika hadi wakati wa mitume, basi kungeweza kujulikana kwake. Hata hivyo, hakuna ishara yeyote inayothibitisha kuwepo kwao, kaka Kanisa lililokuwa mfano, kwa kipindi cha karne kadhaa baada ya kipindi cha Claude. Usemi wa Muston (katika jarida liitwalo Paris, p.xxxii, n. 2) hiyo ilikuwa katika mwaka wa 1096, Urban II aliwaelezea Wavaudois kama ni watu walioathirika na hafundisho ya uzushi, Adeney anasema (katika ukurasa wa 665), kuwa ilikutwa hivyo kimakosa, kadiri ilivyoonekana kuwa hakuna kumbukumbu kwa watu hawa, iliyokutikana miongoni mwa makatazo yake yaitwayo Bulls (cf. Comba p.154). Kuenea kwa mafundisho haya, hatahivyo, kulivunjwa moyo na Waathanasia kwamujibu wa vile ushahidi unaovyoonekana. Ukweli ni kwamba Kanisa la Waamini Utatu liliendelea kuwepo kule kwa kipindi cha karne kadhaa.
Adeney alishikilia kuamini kuwa Waaldens waliyakataa mafundisho ya kujitenga na kujinyima, mafundisho kuhusu toharani na ibada za kuwaombea wafu, na kukataa tafsiri iliyokuwepo juu ya sakramenti ambayo pia ilikuwa ikihudumiwa na makasisi wasiostahili (sura ya 666). Lakini anadhani kuwa mafundisho makamilifu hayajapata kufundishwa bado na nikama yamefichika na hayajajulikana. Matendo ya kidhahiri kuhusu mafundisho ya Kristo, yamejumuishwa kwenye injili zilizoandikwa, na ilikuwa ndiyo kiini chake kikuu, kama ilivyokuwa kwa akina Peter Waldo, mtu ambaye ilidaiwa kuwa jina lake ndio ilikuwa ni chanzo cha wao kuitwa hivyo. Waldo alifariki huko Bohemia mnamo mwaka 1217. Adeney anasema kwamba Knisa la Waaldensia lilikua kwa kupitia mchanganyiko huu wa kazi ya Waldona wa Watu Maskini wa Lyons, na vuguvugu la Arnold wa Brescia, Peter wa Bruys, na ‘Henry wa Cluny’ (kama hapo juu). Kwa hiyo, Waldo aliwekeza utaratibu wake kwa kiasi kikubwa sana kwenye makundi yaliyokuwa yameanza kuwepo kwanza huko nyuma tayari katika Vaudois na mahali pengine popote na kuwapa ujasiri mpya. Vuguvugu la Peter wa Bruys lililojulikana kama Petrobrusians, ndilo linaloelezewa pekee kwenye maandiko yanayosema kinyume chake na Mheshimiwa Peter na nakala yake huko Abelard. Kwahiyo, taarifa hii inaonewa mashaka. Peter alianza kufundisha kwenye parokia au sharika za huko Embrum, Die, na Gap kati ya takriban miaka ya 1117-1120. Alikuwa ni mshambulizi wa imani zilizoota mizizi miongoni mwa watu, aliyefikia hatua ya kuchoma misalaba. Alichomwa moto kwa kushitakiwa kuwa ni muenezaji wa mafundisho ya uzushi miaka ishirini iliyofuatia baadae, huko St. Gilles karibu na Nimes. Alipata wafuasi walioandama mafundisho yake huko Narbonne, Toulouse na katika Gascony. Mtawa wakiume wa Kicluna, Henry wa Lausanne alidaiwa kuwa aliyachukua mafundisho ya Wapetrobrusia mnamo mwaka 1135 na kuyarudisha upya kwa kuyaboresha zaidi baada ya kuuawa kwa ajili ya imani kwa huyu Peter wa Bruys. Mafundisho haya yalihusiana na ubatizo wa watu wazima, na inadaiwa kuwa kikundi hiki kilifundisha kuhusu na kuweka mkazo kwenye umuhimu wenza vifungu vya maandiko matakatifu yaliyopo kwenye Agano Jipya, nk. Utegemezi shirikishi kati ya nyaraka na injili na kukataliwa kwa Agano la Kale. Ni vigumu kuwa ni mpingaji wa mafundisho haya kikamilifu na huku ukiwa unalikataa Agano la Kale. Maagano yote mawili yanategemeana ili kutumiwa na wafundishaji wa ukweli wa neno na kukanusha mafundisho ya uwongo.
Inadaiwa sana kuwa pia walikataa kushiriki Meza ya Bwana na mapokeo ya Ekaristi, kwa kuwa marudio ya dhabihu yalikuwa sio rahisi. Waliamini kuwa Kanisa lilikuwa ni ile jumuia na sio majengo na walidhani kuwa majengo ya Makanisa yalipaswa kuharibiwa au kubomolewa kabisa. Madai kuhusiana na watu hawa, yanabakia kwa maadui zao. Nukuu zilizoko kwenye kitabu cha maarifa cha Kikatoliki, maarufu kama Catholic Encyclopedia kilichoandikwa na N.A. Weber (usomapo art. Petrobrusians, Vol. II, p. 781) ni mwandishi yule yule aliyeandika makala ya Waaldensian. Mawazo yaliyokutikana katika maeneo haya yalidaiwa kuwa hewani. Hata hivyo, jarida la ERE (katika makala yake ya Wapaulician na Waaldense) inafanya ionekane kwamba kulikuwa na maendeleo ya jumla ya mawazo kwa Ulaya yote kutoka pande za Mashariki. Tumeona kwamba chanzo hiki ni cha Wapaulician, ambao waliweka makazi yao huko Thrace. Bila shaka Makanisa haya yalifungamana na wafadhili wa pande za magharibi.
Waaldensian Wasabato au Wasabatati
Waaldensian,au Wavallense, walidaiwa kuwa walikuwa wamepatiwa jina la Insabathas au Insabbatati, kwa sababu hawakufanya maadhimisho ya ibada siku nyingine iwayo yote, ila ni siku ya Sabato peke yake. Ndio maana waliitwa kuwa ni Wainsabathas, kana kwamba hawakuwa wanatunza maadhimisho ya Sabato (kwa kuwa hawakuwa wanaadhimisha siku ya Jumapili), [kwa mujibu wa jarida liitwalo Watangulizi wa Luther, au Luther’s Fore-Runners, pp. 7-8 (ambalo kwa makosa lilitaja na kuona pia Gui, yaani Manuel d’Inquisiteur)]. Waaldensian hawakulipata jina lao toka kwa Peter Waldo ila zaidi sana ni kwamba walirudishiwa kwa namna ya kumbukumbu. Wanahistoria wa Kikatoliki huandika kana kwamba wanataka kutoa mkazo kwamba Waaldensian walikuwa ni mageuzi na kujaribu kubuni kuonyesha msukumo waliokuwanao, Wakatoliki, walikuwa na mamlaka ya kitume juu ya Makanisa mengine yote mbayo hatimaye yalikatiliwa mbali.
Propaganda hii hatimaye ilichukuliwa pia na baadhi ya Waprotestant kwa sababu ya tabia asili ya Kihistoria ya Wavallense, ambao walikuwa Wahafidhina katika imani ya Washika-Sabato. Peter Allix anasema hivi kuhusiana na watu hawa:
Sio kweli kuamini kuwa Waldo alitoa jina hili kwa wakazi wa mabondeni; waliitwa Waaldense, au Wavaudes, siku kabla wakati wake toka mabondeni walimokuwa wanaishi (kwa mujibu wa jarida liitwalo Kanisa la kale la Pidmont, au kwa Ligha ntingine, Ancient Church of Pidmont, Oxford, 1821, p. 182).
Allix anaendelea kwa kusema kuwa:
Baadhi ya Waprotestant, kwa mazingira kama haya, wameangukia kwenye mtego ambao uliandaliwa kwa ajili yao…. Ni uongo kabisa, kusema kwamba makanisa haya kamwe hayakuanzishwa na Peter Waldo…. Ni kinyume kabisa na ni kughushi (yamo kwenye jarida hilo hilo, uk. 192).
William Jones (katika jarida lake la Historia ya Kanisa la Kikristo, kwa Kiingereza, History of the Christian Church, Vol. 2, p.2) anasema kwamba yeye:
Alikuwa anaitwa Mvaldu au Muwaldo, kwa sababu alipokea mawazo yake ya kidini, kutoka kwa wakazi wa mabondeni.
Wakati ambapo mtu anapotathimini ushahidi wa kimaandiko matakatifu na maandishi ya watetea dini wa Kikatiliki kama vile akina N. A. Weber, utakuta kuwa hakuna ushahidi unaotolewa zaidi ya ukweli wa kwamba, mabarbe wawili hawa (maana yake ni Wajimba au Wazee) wa Waaldensian waliitwa Wavallense kwa mara yake ya kwanza, na Raymond wa Daventry kwenye matamshi yake ya shutuma mnamo mwaka 1180 (kwa mujibu wa jarida la Adversus Vallenses et Arianos). Adney ananakili hii kwenye kazi yake lakini Weber hajaweka hili. Inaonekana kwamba neno Vallenses lilichukuliwa kutoka kwa Waldo katika siku zake. Hatahivyo, hii haina maana yeyote kwa kweli, kama jina lenyewe linavyoashiria kuhusu mabonde na sio kwa Waldo. Hivyo basi wakati madai yakifanywa na Weber, na inaonekana pia kuwa na Adeney, mstakabala wake waweza kukataliwa ukaonekana kama ni dhana tu isiyo sahihi.
Inaonekana kuwa kuwekwa kwa mpangilo upya katika mji wa Milan, kulisababishwa na kuingia kwa msimamo wa hawa Wasabato au Wasabbatati kama walivyojulikana waliotokea pande za Austria, na pande za kaskazini-mashariki, waliopewa kile tunachoweza kugawana pamoja na vuguvugu hili. Kwa hiyo, uanzishwaji wa Chuo huko Milan na kwa chanzo kikubwa huko Austria ili kutuliza ama kuzima jaribio lolote la kuanzilishwa kwa ufuasi wa Waldo. Kwa kweli, Blair katika kitabu chake kijulikanacho kama Historia ya waaldense ama History of Waldenses (Vol. 1, p. 220) anasema kama tunavyo mnukuu:
Miongoni mwa makabrasha, tuliyonayo ya watu walewale, matarajio kuhusu Amri Kumi za Mungu yaliwekewa siku zake na Boyer takriban mwaka 1120. maadhimisho ya Sabato kwa kuacha kufanya kazi za kidunia kulijumuishwa.
Kwa hiyo, Waaldensian walikuwa ni watunza-Sabato na Waunitariani Waliobobea kiimani ambao kwa siku kabla ya Waldo walikuwa kwenye ulengwa. Kwa mujibu wa Dugger na Dodd, kwenye jarida lao la Historia ya Dini ya Kweli ama A History of the True Religion, (3rd ed. Jerusalem, 1972, p. 224 ff) linasema kama hivi tunavyo nukuu:
Benedict katika historia yake ya Wabaptisti anawataja Waaldense kwamba: ‘Tayari tumeshajionea wenwe kutoka kwa Claudius Seyeseel, askofu mkuu wa mteule wa papa, ya kwamba kile ambacho Leo ameshutumu ni pamoja na uanzishaji wa mafundisho ya kizushi ya waaldensian kule mabondeni, katika zama za Costantine Mkuu. Wakati vipimo hivyo vikamilifu vikianzishwa na Mfalme Honorius akiwapinga wale wanaowabatiza watu upya [yaani Waanabaptisti], walikiacha kiti cha utajiri na uweza, na kutafuta mapumziko ndani ya nchi, na kwenye mabonde ya Piedmont (Italia) ambayo kwa hakika ni sehemu yake ya mwisho, yakifanyika kuwa ni makimbilio yao yaliyokinyume na shuruti za mfalme’.
Rainer Sacho, mwandishi wa vitabu na majarida au makala wa Kikatoliki, anawasimulia waadense kuwa: ‘Hakuna kikundi cha kidini kilicho cha hatari zaidi sana kama walivyo Waleonist, kwa sababu tatu zifuatazo: kwanza kabisa ni kwa sababu ni cha zamani zaidi kuliko kingine kiwacho chote, wengine hudiriki kusema kuwa ni cha zamani sana kupita hata umri wa Slyvester, wengine husema kuwa ni cha siku nyingi zaidi hata kuliko hata mitume wenyewe. Sababu ya pili ni kwamba, kimefanikiwa kuenea kimafundisho kwa ujumla, kiasi kwamba hakuna chi ambayo hawajafanikiwa kufikisha mafundisho yao. Na sababu ya tatu ni kwamba, wakati ambapo vikundi vingine vinaonekana kuwa vinavunja maagizo kutoka kwenye mandiko matakatifu au kukufuru, hawa wanaonekana kwa dhahiri kabisa kuwa ni wenye mioyo ya huruma, wakiishi maisha yasiyo na mashaka na yenyehaki mbele za macho ya watu waliacha kuamini kitu chochote kimhusucho Mungu jambo ambalo si jema.’
Sacho anakiri kuwa waliendelea kustawi wakifanikiwa kwa kipindi cha takriban miaka mia tano mapema sana kabla ya kipindi cha Peter Waldo. Masalio yake yaliruhusiwa pia na Gretzer, mjesuit, ambaye aliandika makala kuwapinga. Crantz katika jarida lake lisemalo: Historia ya “Ndugu zetu Wapendwa Waliounganika,” anaongelea migawanyiko ya Ukristo kwa maneno yafuatayo: ‘Wakristo hawa wa zama za kale huweka kumbukumbu za siku zao kuanzia mwanzoni mwa karne ya nne, kipindi ambacho Leo katika mageuzi makuu ya kidini chini ya Costantine Mkuu, alipinga mabadiliko yaliyotakiwa kufanywa na Sylvester, askofu wa Roma.
Kwa mujibu wa Allix tunaona anavyosema kuwa:
Wana Mageuzi wanaamini kuwa Kanisa la Waaldensian lilianzishwa mnamo mwaka 120 AD, tarehe ambayo walipita kutokea kwenye mafundisho ya baba hadj mwana mafundisho waliyopokea kutoka kwa mitume. Biblia ya kilatini ya Kiitalia ilitafsiriwa kutoka Lugha ya Kiyunani kwa mwaka usiozidi ule wa 157 AD. Tunawiwa na Beza, aliyejulikana kama ni mshiriki mwenza wa Calvin, kwa imani inayoendana na Matamko ya Kanuni ya Imani ambayo Kanisa la Kiitalia lilihesabu kuanzia mwaka 120 AD. (kwa mujibu wa jarida la Allix lisemalo Makanisa ya Piedmont, au Allix Churches of Piedmont, 1690, adn, p. 177 na la Wilkison lisemalo Biblia yetu Iliyothibishwa Yenye Mamlaka, au Our Our Authorized Bible Vindicated, p.35 na jarida la Utambulisho wa Scrivener, au Scrivener’s Introduction, Vol. II. P. 43, cf na lile la Dugger na Dodd lisemalo Historia ya Dini ya Kweli, au, A History of True Religion, pp. 224-225).
Mbinu tendaji katika mwaka 120, inauthabiti na upelekaji wa wanafunzi wa Polycarp kutoka Symirna (na Efeso) kama tilivyoshughulika kujifunza kuhusu mateso ya Kanisa la Lyons, chini ya marcus Aurelius katika mwaka 177, ambapo Phontinus, mwanafunzi wa Polycarp, aliuawa kwa ajili ya imani ya kidini, na sehemu ya taarifa yake kupelekwa kwao Symirna. Makanisa huko Gaul yalikuwa chini ya uangalizi wa Baraza la kikanisa la Milan kwa kipindi cha karne kadhaa, kama ilivyojijenga ndani yake hadi uingiliaji wa papa ulipotokea.
Dugger na Dodd pia wananukuliwa (katika ukurasa wa 226) wakisema kwamba:
Atto, askofu wa Vireulli, aliwalalamikia watu wa aina hii miaka themanini kabla [kabla ya mwaka 1026 AD].na kulikuwepo na wengine wengi kabla yake, na kuna sababu kubwa sana za kutupelekea kuamini kwamba wakati wote walikuwepo nchini Italia (twasoma haya kwenye jarida la Jones liitwalo Historia ya Kanisa au Church History, p. 218).
Kwa hiyo, uanzishwaji wa chuo cha Waaldensian huko Milan, ni mbinu za kueneza utambulisho wa mambo yao kwakutumia njia ya asili. Dugger na Dodd waliendelea kumnukuu Mosheim akisema kwamba:
Huko Lombard, mji uliokuwa ni makao makuu ya kimakazi ya wafundisha mafundisho ya uzushi wa Italia, walipanua kikundi kimoja cha kidini, ikijulikana kwa sababu ambayo sitaweza kuitaja, kwa kukomesha imani ya Wapassaginian… Kama ilivyo kwa vikundi vilivyotajwa tayari, walikuwa na ukwepaji wa kina kutoka wanafunzi na uweza wa kimamlaka wa Kanisa la Rumi, lakini walitofautiana na mafundisho ya misingi ya kanuni ya imani kimadhehebu mengine ambayo yalikuwa ni ya pekee ya aina yake kwa jinsi yalivyokuwa kwa jinsi yake yenyewe.
Suala la kwanza lilikuwa ni juu ya wazo la kwamba maadhimisho au kuzishika sharja za Musa kwa kila kitu isipokuwa kwa sheria za sadaka au dhabihu, kulikuwa ni jambo la lazima kwa Wakristo: kwa matokeo ambayo kwayo yatakuwa… Walijiepusha na ulaji wa nyama zilizo najisi, matumizi ya vitu vilivyokatazwa kwa mujibu wa matarajio ya ubanamatumizi wa mafundisho ya Musa, na waliadhimisha Sabato za Kiyahudi. Fundisho lingine la pili lililoweka tofauti kati ya vikundi hivi vya kidini liliendelea mbali kutoka kwenye upjnzani hadi kwenye mafundisho ya uwepo wa nafsi tatu kwenye asili ya uungu (jarida liitwalo Eccl. Hist., Cent 12, Part 2, ch. 5, Sec. 14, p. 127. kama lilivyonukuliwa na Dugger na Dodd, kulitiliwa mkazo).
Dugger na Dodd wanafika mbali kwa kusema kuwa:
Kwamba Cathari haikurudi na kushika maadhimisho ya Sabato ya kale, ilithibitishwa na maadui wa Kiroma. Dr. Allix alimnukuu mwandishi maarufu wa vitabu wa Kanisa la Kirumi wa karne ya kumi na moja kuhusiana na mambo matatu yanayoweza kusababisha mafundisho ya kiuzishi kwa Wacathari, kwa Wapassiginiani, na Waarnoldista, Allix anasema kwa ajili ya huyu mwandishi wa Kirumi kwamba:-
‘anaweka jambo hilo chini kama ni mojawapo ya maoni au mitazamo yao, ‘kwamba Sheria za Musa zinatakiwa ziadhimishwe kwa mujibu sawa na waraka usemavyo, na kwamba utunzaji wa Sabato… na maadhimisho mengine yaliyoruhusiwa, yalitakiwa yafanyike na kuchukua mkondo wake. Walishikilia pia kuamini kuwa Kristo, Mwana wa Mungu, hayuko sawa na Baba, na kwamba Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, watatu hawa… sio Mungu mmoja na kiini kimoja na salio, kwenye makosa haya, walihukumu na kushutumu madaktari wote wa Kanisa…(jarida liitwalo Historia ya Kanisa, ya Kanisa Makanisa ya kale ya Piedmont, au Eccl. Hist. of the Ancient Churches of Piedmont, pp. 168-169, cf Dugger and Dodd, pp. 227-228).
Kwa hiyo, inaweza kuonekana kwamba Wacathari, Waaldensian na Wapassigiani, walikuwa ni matawi ya kundi hili hili. Wangeweza kutofautishwa, kwa sababu hawakuwa kamwe kwenye orodha ya Makanisa yenye mafundisho ya uzushi. Waliweka utaratibu wao kwa kufuata misingi na mlolongo wa Agano Jipya na hii ndio mojawapo ya sababu zilizowafanya wasiwezekane kufutilia mbali. Na zaidi sana wanaonekaaa hasa hasa kuwa ni Watu tegemezi katika imani na waliojitoa katika imani ya Unitarian. Kwahiyo, Makanisa ya kwanza yaliyokuwepo barani Ulaya yalikuwa hayakuwa ya ama ya Wale wenye kuamini uungu wa miungu miwili (Waditheist/Binitarian) au Wenye kuamini mafundisho ya Utatu (Watrinitarian), lakini walikuwa ni Wenyekuamini uungu wa Mungu mmoja, yaani Waunitarian.
Dugger na Dodd pia wananukuu (kwenye kurasa za 228-229) kwamba walikuwa na jina lingine ambalo ni Wapateriane, kama walivyojulikana na kuitwa huko Liman, ambako lilitumika kwa mara ya kwanza, ilijibiwa kwa lugha ya Kiingereza sawa na ushenzi au kitu cha kawaida na ilitumika katika utaratibu wa watu wa hali ya chini, ambao waliojipatia riziki zao kwa kufanya shughuli duni. Dugger na Dodd wanadai kuwa Gazari ilikuwa ni uchafuko wa Wacathari, au Wapuritan, hatahivyo kwa vyovyote vile, kuna mfano jinsi nyingine ya kufanyia matendo. Hawadiriki kwa vyovyote vile kuwakilisha maswali kuhoji ushawishi wa Wakazari au Wakhazari, kama ionekanavyo hapo chini.
Bilashaka tunaweza kusema kuwa Waaldensian walikuwa ni imani ya Walioegemea ambao walikuwepo mapema kabla yake na hadi kwenye takriban mwaka 1179 mapema tu kabla ya kuanzishwa kwa Baraza la Lateran (hili halikugusiwa hata na Weber). Mabarbe zao wawili yaani kina Oliver na Sicard, walijikuta wakiingia kwenye mgogoro na askofu Montperoux katikati ya miaka ya 1175-1176 na miaka miwili au mitatu baadae, Papa Alexander III alimtuma caldinari wa mt. Chriysogone, aliyeitwa Henry wa Citeaux na Reginald, askofu wa Bath, kasha wakati akiwa njiani kuelekea kwenye Baraza la Lateran akisindikizwa na mtawa mwanaume aliyeitwa Walter Mapes na kasisi Raymond wa Kibaimia, ili atahiniwe na John wa Bellesmains, askofu wa Poitiers. Kasha wakaelekea hadi Narbonne ili wakafahojiwe na Bernard wa Fontcaude, chini ya baraza la kirais la kasisi Mwingereza aitwaye Raymond wa Daventry. Alikuwa ni kasisi huyu, Raymond wa Daventry, aliyelitumia kwa mara ya kwanza jina la Vallences au Waldenses. Hivyo walipewa jina na washitaki au maadui zao, kwa jina la mmojawapo wa viongozi wao. Mabarbe wawili walishutumiwa kwa kutuhumiwa kuwa walikuwa ni wahusika wa kufundisha mafundisho ya uzushi na huyu Raymond wa Daventry katika mwaka wa 1179, ambaye aliendelea na Baraza la Lateran. Tendo la kukiita kikundi hiki kwa majina ya viongozi wao wakuu limekuwa ni tendo la kawaida kwa kipindi cha karne kadhaa na kupewa muonekano wa uongo kama mkondo wa mawazo na makusantiko ya wahudhuriaji.
Mnamo mwaka 1180, Bernard wa Fontcaude aliandika kitabu alichokipa jina la Adversus Vallenses et Arianos (tazama jarida liitwalo Gay. Hist. des Vaudois, p. 16, n. I na pia Adeney, hichohicho uk. 667). Hapa Adeney anasema hivi:
Inaonekana kwamba majadiliano haya yanatokana na umoja uliopo kati ya Wapetrobrusiani na Wahenriciani na Watu Masikini wa Jimboni Lyons. Kwa takriban muda huo huo wafuasi wa Waldo waliungana na Waarnauldist wa Lombardy. Kwa hiyo Waaldensiani wa Ufaransa na Italia waliunganika, na muungano wao ulipatanguvu kutokana na mateso. Nia ya kutengwa nje ya ushirika wa imani na Baraza la kidini la Verona iliwaweka sawa wafuasi waliobakia wa Waldo na kuwatoa nje ya Lyons na kuwapeleka kwenye Jimbo, kwenye Mabaraza ya kifalme, na kwenye mabonde ya Piedmont, Lombardy, na hata baadhi yao Ujerumani. Kwa hiyo wengi wao walifanya kama alivyokuwa Innocent III alituma watumishi wake ili waende kuwakomesha hawa mnamo kwenye miaka ya 1198, 1201 na 1203
Bilashaka kabisa kwa namna yoyote ile kuamini kuwa sisi tunashughulika na Watutegemezi wa imani na mafundisho Wanaoamini juu ya Mungu mmoja yaani Waunitarian, ambayo ililinganishwa na kama na imani ya Waariani. Katika kipindi cha ukandamizaji cha mwaka 1203, watesi hawa ikiwa ni pamoja na askofu wa Kihispania na Dominic (anayeitwa mtakatifu) mwanzilishi wa shirika la Wadominicani, ambaye hatimaye alipata nafasi kwenye Baraza la kidini la Hukumu pamoja na Wabenedictine. Waliandaa mafanikio ya jinsi ya kushinda kwenye malumbano ya yaliyoishia takriban mwaka 1207, wakati mjumbe Peter wa Chateauxneuf alipouawa. Miaka miwili baadae, Papa alitangaza vita ya kidini. Kwa wazi kabisa, Adeney anaonekana kuhusishwa kuwemo kwenye vita hii ya kidini kama ni vita, lakini kwa kweli Waaldensiani ndio walikuwa hasa ni shabaha au waliolengwa kwenye vita hivi kwa maana ile ile. Mnamo mwaka 1210, Mfalme Otho alimuamuru askofu mkuu wa Turin kufafukuza Waaldense watoke kwenye diocese yake, na mnamo mwaka 1220 Muadhama Statutes wa Pignerol aliwakataza wakazi wake wote kuwapokea au kuwapa hifadhi watu hawa. Baadhi yao walikimbilia huko Picardy, na Philip Augustus aliwafukuza wapotelee mbali hadi walifika Flanders. Baadhi yao walikuja Mayence na Bingen, ambako miongoni mwao 50 walichomwa moto mnamo mwaka 1232. (jarida la Adeney hilo hilo linasema).
Walikuweko kwenye siku za mapema sana katika Hispania, wakishutumiwa na kushitakiwa Mabaraza ya Makanisa na kuharakishwa na Wafalme watatu miongoni mwao. (inasemwa na jarida hilohilo).
Kipindi hiki kiliishia kwa kuundwa kwa Mabaraza ya Hukumu na vita ya kidini ya Waalbigensiani, ambayo ilienea Uhispania kote ikitokea Ufaransa (tazama hapo chini). Watu hawa walikuwa ni jumla ya makundi tofauti ya Wakristo. Na kwa kweli baadhi ya vikundi hivi sio tu kwamba vilionekana kuwa ni vya Watunza-Sabato kwa zama hizi za mwanzoni, lakini pia waliteswa kwa ajili ya kufanya maadhimisho ya Siku nyingine Takatifu zilizoamuriwa katika Biblia. Jambo hili ni lazima lihusishwe na kuwekwa kwa makatazo kuhusiana nayo, kukihusishwa na ukiri unaotokana na mateso makali. Ili kwamba wanayohitaji kuyachukulia kwenye mashitaka wafanikiwe kuwa na ushahidi nayo. Hata hivyo, kuna ushahidi wa moja kwa moja kwa baadhi ya Makanisa ya Wahungari (kwa mfano). Ni muhimu kujua vita vinavyoongelewa hapo juu kama vilivyokuwa vimeanzia mnamo mwaka 1209, kwa kweli ilikuwa ni ya Waalbigensian, ambayo iliishia hadi ulipofika mwaka 1244 na iliwalenga wale waliokuwa wanatuhumiwa na kwa kweli waliteswa kikatili kabisa pasipo kuwahurumia. Mamlaka tawala iliamuru kupigwa mijeledi bila ya huruma na kuchochea chuki kuu imwaangukie mtu awayeyote miongoni mwao wale walioitwa kuwa ni waenezaji wa mafundisho ya uzushi na kasha waletwe mbele ya Baraza la Kidini la Mahojiano na hukumu (tazama kitabu cha mwandishi C. Roth kijulikanacho kama Baraza la Kidini la Mahojiano na Hukumu, maarufu kama C. Roth, Spanish Inquisition, pp. 35-36 kwa ufafanuzi zaidi). Mwelekeo wa Waaldensia kwa kipindi hicho hicho, unaonyesha kuwa tulikuwa tunashughulika na vikundi hivi vyote vya watu kwa mgawanyo unaolingana kama wa Waalbigensia. Waaldensia walikuwa ni wahubiri walioitafsiri Biblia moja kwa moja yaani kama ilivyoandikwa, ambao walikuwa ni Wafuasi-tegemezi ambao walipewa jina (kimakosa) wakaitwa Waarian.
Waumini waliokataa kufuata mafundisho ya Utatu katika Uhispania, walitambulikana na kukubalika na Wayahudi kwa ajili ya tabia na mwenendo wao ulivyokuwa yaani kwa ajili ya kukataa kwao imani ya Utatu, ingawaje kwa sheria ya Kibaraza za mahojiano ya imani ya dini iliyoletwa baadae mwaka 1519 na Andreas de Palacio, ilisababisha Wakristo kwa kiasi kikubwa wagawanyike au kushindwa kabisa (angalia kitabu cha Roth. Uk. 77 kuhusu makato haya). Mahali popote walipokuishi Waaldensia katika nchi ya Utaliano, baada ya marejesho ya imani kwa upande mwingine wanaonekana kana kwamba walianza kuwa ni wafuasi wa mafundisho haya ya Utatu na historia yao kama ilivyoandikwa na Waprotestant na kwa kiasi fulani inaonekana kujitetea kama inavyoonekana kupingana na historia ya siku za mwanzo ya tafsiri ya moja kwa moja kutoka katika Biblia.
Mnamo mwaka 1237 Papa Gregory IX alifanya mambo yafuatayo:
Alipeleka tangazo la amri ya makatazo kwa askofu mkuu wa Tarragona lililosababisha watu kumi na tano miongoni mwa wale waliojulikana kama ni wafuasi wa mafundisho ya uzushi wachomwe moto, Mfalme Ferdinand kwa mikono yake mwenyewe alishiriki kukoka kuni ili kuongezea ukali wa moto. Kwa wakati wake uliopangwa, Waaldeansian hawa wa Kihispania walikomeshwa (soma kitabu hicho hicho hapo juu cha Adeney).
Waaldensia walizidi kuenea sehemu nyingi za Ujerumani, ambako Makanisa yao yalipeleka wawakilishi wao ili kugombea vyeo au nafasi za kuhudumia kwenye Chuo cha Waadensian kilichokuwa huko Milan. Mkuu wa chuo alikuwa ni John wa Ronco ambaye aliteuliwa kushika wadhifa huoa kama cheo cha maisha, pamoja na kukusekana kupata kibali na Waldo.
Ilikuwa ni kwa ajili ya ukweli huu ambao ulisababisha mgawanyiko kati ya kundi la Wafaransa na lile la Wataliano na Kundi jingine la Wajerumani. Upande wa Lombards walimweka mchungajii wao mkuu (proepositus). Yeye pamoja na watumishi wengine wakishikilia nyadhifa zao kwa vipindi vya maisha yao yote, wakati ambapo Waldo na Waaldense Wafaransa waliokuwa chini ya mamlaka yake, walichagua viongozi wao kwa kila mwaka ili wahudumu kwenye ibada ya Ushirika wa Meza ya Bwana wakitumika kama wachungaji. Kwa hiyo, tunaweza kuanzisha kile tunachoweza kukifanya kwenye makundi yaliyokuweko kwenye karne hii ya kumi na tatu ambacho ni kushiriki Ushirika wa Meza ya Bwana kwa mtindo wa kila mwaka mara moja. Dhana au wazo la kudhania kuwa huenda walikuwa watu hawa ni washika maadhimisho ya Jumapili halionekani kuwa na maana au kushawishi mawazo na kuaminika.
Tatizo kubwa lisilo la kawaida lililojitokeza kuhusiana na jambo hili, lilikuwa ni kuendelea kuwepo kwa Waalbigensia kwa upande wa kaskazini na huko Ufaransa upande wa Alps. Upande wa kusini na mabonde ya Italia kulikuwa kunakaliwa na Waaldensian. Kutokana na migawanyiko inayoonekana hapo juu inawezekana sana kusema kwamba majina yaliyotolewa na Wakatoliki kuwaita wale wanaoshughulika na mabaraza ya mahojiano inaonekana kuwa na ukweli kuhusu wao wenyewe. Makatazo yaliyokuwepo huko Hispania hata hivyo, yanatuashiria kuwa na sisi tunafanya kitu kile kile kama ilivyokuwa ikifanywa na kikundi hiki cha kidini. Mgawanyiko uliojitokeza baadae ungaloweza kudhaniwa kuwa ni wa tofauti na hali halisi, ni wakati kikundi hiki kilipoamua kuwa ni cha mrengo wa Kiprotestant unaoamini imani ya Utatu. Hatimaye Bohemia alifariki miaka 40 baada ya kufariki kwake Waldo kwa mujibu wa mahakimu waliokuwa wanasimamia mabaraza ya kidini ya Passau, alikuwa na vituo alivyoviita kuwa ni viota 42 vilivyoitwa kuwa ni vituo vya kufundishia mafundisho ya uzushi (kwa mujibu wa Adeney, op. cit). Mfalme Octakar aliamuru yawepo mateso ambayo yalikuwa ni mabaya sana chini ya Papa Benedict XII mnamo mwaka 1335. Kuinuka kwa vuguvugu la Wahussi kulisababisha mchangamano wa namna ileile kwa makundi mawili wakitumia jina la Watabora. Adeney anaamini kwamba aliyekuwa maarufu zaidi kuliko wote ni barbe Frederic Reiser. Baada ya miaka 25, miongoni mwa Waaldensia wa Bohemia na Austria, alikufa kifo cha kuchomwa moto huko Strassburg mnamo mwaka 1458.
Kwa hiyo, kuna angalau vikundi vine kwa zaidi ya nchi nane, ambavyo baadhi yake vilikunganishwa na Waprotestant. Walikuwepo Waaminitegemezi, au Waunitaria, katika Austria katika karne ya kumi na tatu na Mahakimu wa Krems waliitenga mitaa 36 katika mwaka 1315, na kuwaua kwa kuwachoma moto mashahidi wafia dini 130. Askofu wa Neumeister aliuawa kwa kuchomwa moto akichukuliwa kama ni miongoni mwa watu hawa wafundishaji wa mafundisho ya kiuzushi huko mjini Vienna. Alisemekana kuwa alisikika akitanga kwamba kulikuweko na takriban Waaldensian 80,000 kwenye mapambizoni mwa Austria mwishoni mwa karne ya kumi na nne kulitokea mauji makuu na ya kikatili sana huko Syria. Kulikuwa na na mikakati ya makusudi iliyoratibiwa vizuri iliyopangiliwa huko Italia yalitokea Austria ambako wamisionari walisafiri wakijifanya kama wafanya wachuuzi wa biashara ndogondogo (yameandikwa kwenye kitabu hiki hiki cha Adeney). Vuguvugu hili lilikuwa na chuo huko Milan kipindi ambaho Waldo akiwa hai, bado hajafariki. Kutokana na hatua hizi ni vigumu kudai, kuwa kama vile Adeney alivyokuwa, kwamba Waamini-tegemezi wa Austria walikuwa ni Waaldense, ambao kwamba wakipelekewa wahubiri au uinjilist toka Austria kwenda Italia. Askofu aliokekana kabisa kuwa ni wakundi moja hilohilo, aliyeitwa baadae Waldense. Kundi hili pia liliitwa ni Wasabbatati au Washika-Sabato na pengine waliitwa Insabbatati ikiwa na maana ile ile, ambao ilidaiwa kuwa walichukuliwa kutoka kwenye miti iliyoitwa sabots au kwenye viatu vya siku za kale zilizoitwa talawanda, ambavyo vilivaliwa. Ni vema sana kufikiri kwamba kuharibika kwa mitazamo yao kuhusu Sabato, kulibadilika na kuwa ni maneno matupu. Hii hasa ilikuwa ni maendelezo ya maneno au usemi usemao Sabotiers yaani Watunza Sabato na kisha waliitwa Wasandaliati ikimaanisha vilevile. Weber (katika jarida lake liitwalo C.E. art. Waldenses, Vol. XV, p. 528) ikishindwa kugundua tofauti ya mabadiliko ya Lugha kati ya maneno na kwa kweli kuyachanganya kwenye maagizo yao ili kuhakikisha nafasi yake. Pia anadai kwamba vikundi hivi vya imani vilichukuliwa kutoka kwa Waldo, vikidharau karibu kwa sehemu zote ushahidi uliotajwa na Adeney. Huenda taarifa zaidi ilipatikana kwa Adeney, lakini mtafaruku uliokuwa ndani ya kazi ya Weber inaonekana na inaeleweka kutolewa katika historia.
Waaldense walikatazwa kuhubiri na askofu mkuu na wanadaiwa kuwa walikata rufaa kwenye Baraza la tatu la Lateran, chini ya Alexander III, ingawa walishutumiwa, kutoka juu, mbele ya Baraza mnamo mwaka 1179. Walitathminiwa kwenye mitihani. Inapaswa ikumbukwe, kwa siku hizo kwamba katika utaratibu wa zama za kati ulitoa uhakikisho kuwa kasyi ilikuwa ni mali ya mabwana zao, chini ya maongozi yaliyotoka Roma na kwamba haikuwa rahisi kushikilia imani iwayo yote, sio kwa kufuata mujibu wa Roma. Kwa hiyo walitakiwa kujitokeza kama walivyoambiwa, ingawaje hawakuwa na makubaliano na madai ya Roma. Si kwa kufanya hivyo, walipaswa kuuawa kwa kuchomwa moto kwa namna iwayo yote.
Mgawanyiko mwingine uliokuwa muhimu sana kuwemo miongoni mwa Waaldensian, waliotokea toka kwenye mafundisho ya Waaldensian Wataliano, kwamba sacrament zilizohudumiwa na makasisi wasiostahili zilikuwa hazina madhara yoyote. Wafaransa hawakukubaliana na mtazamo huu. Wataliano wazilikataa sacrament zote zilizotolewa na makasisis wa Rumi na kwa wakati huo huo kusisiza mshikamano wa karibu na mafundisho ya Agano la Jipya. Migawanyiko hii ilijadiliwa katika halmashauri kuu iliyokutana mwezi wa tano au Mei 1217, mwaka aliofariki Waldo (kwa mujibu wa kitabu kilekile cha Adeney). Matawi mawili ya Waaldensian walianza mawasiliano kwa wakti wote,